Advertisements

Saturday, May 13, 2017

SHIRIKA LA AFYA DUNIA LATANGAZA MLIPUKO WA EBOLA DRC

Shirika la Afya Duniania (WHO) limetangaza kuwapo kwa mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Mtu apataye mmoja amefariki baada ya kupata virusi vya Ebola kaskazini mashariki mwa DRC kwa mujibu wa WHO.

Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeifahamisha WHO kupitia twitta vipimo vya maabara vimebaini mtu huyo alikuwa na virusi vya Ebola.

Zaidi ya watu 11,000 walifariki dunia kwa ugonjwa Ebola katika mataifa ya Afrika Magharibi mwaka 2014-2015, wengi wakiwa wa nchi za Guinea, Sierra Leone na Liberia.

No comments: