Advertisements

Thursday, June 8, 2017

Bajeti Kuu ya Serikali Kusomwa Leo

Nchi  za Afrika Mashariki ikiwamo Tanzania zinawasilisha bajeti zao kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango anatarajiwa kuwasilisha bajeti hiyo bungeni leo mjini Dodoma  kuanzia saa 10 kamili jioni.

Kabla ya kufanya hivyo, asubuhi Dk Mpango atawasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi ya nchi, ambayo itajikita katika kueleza mipango ya maendeleo kwa mwaka ujao. 

Kwa mujibu wa ratiba ya Bunge la Tanzania katika Mkutano wake wa Saba wa Bunge la Bajeti, wabunge watatumia kesho kusoma na kutafakari hotuba hiyo.

Kuanzia Jumatatu ijayo Juni 12 hadi Juni 20, mwaka huu, wabunge watajadili Taarifa ya Hali ya Uchumi na Bajeti ya Serikali kwa siku saba kabla ya jioni ya Juni 20, mjadala kuhitimishwa kwa upigaji kura ya wazi.

No comments: