Advertisements

Thursday, September 21, 2017

GEREJI BUBU KUBWA YA KUHUDUMIA MAGARI MIKOCHENI YAFUNGWA KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

Naibu Waziri  Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina(kushoto) akimsikiliza mtaalam  Bw. Filbert Mdonko, kutoka katika kiwanda cha Intergraded Steel Limited kilichopo katika eneo la viwanda Mikocheni Dar es Salaam namna ambavyo Mtambo wa kusafisha Majitaka unavyofanya kazi.
 Sehemu ya eneo la Garage iliyofungwa kwa uchafuzi wa mazingira katika eneo la viwanda Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano a Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, akiongea na kuonyesha maji machafu na yenye sumu yaliyotuwama na maji hayo yanayotoka viwandani katika eneo la Mikocheni Jijini Dar es Salaam alipoendelea na ziara yake ya ukaguzi wa viwanda na utekelezaji wa Sheria ya Mazingira leo.

Na Evelyn Mkokoi – Dar Es Salaam
Garage kubwa yenye kutoa huduma kwa magari ya aina mbalimbali iliyopo katika eneo la mtaa wa viwanda mikocheni jijini Dar es Salaam imefungwa kwa kile kinachodaiwa ni kukikuka sheria ya mazingira na kanuni zake kwa kuharibu mazingira kwa kumwaga mafuta machafu,  kutupa vyuma chakavu na kutelekeza  magari  yaliyochoka.
Hatua Hiyo imechukuliwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Afisa Sheria Mkuu wake  Bw. Vincent Haule, ambapo Bwana Haule Alisema kuwa Garage Hiyo ambayo Mmiliki wake hakutambulika Mara moja inatakiwa kusimamisha shughuli zote za uendeshaji katika eneo hilo ndani ya siku saba pamoja na kuondoa magari yote.
Bw. Haule aliongeza kwa kusema kuwa Mmiliki wa Garage hiyo anatakiwa kufuata taratibu za serikali kwa kupata vibali vyote vya uendeshaji ikiwa ni pamoja na kibali maalum kutoka NEMC.
Baada ya kutozwa faini ya shilingi milioni 10 kwa kiwanda cha Bidco kinachotengeneza bidhaa za sabuni na mafuta ya kula na kutakiwa kuilipa faini hiyo ndani ya wiki mbili, Naibu Waziri Ofisi ya Makami wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, alisema viwanda vinavyochukuliwa hatua kwa uchafuzi wa mazingira vinatakiwa  kutii maagizo ya serikali.
 Mpina pia alitoa maelekezo kwa Manisapaa ya Kinondoni ambapo aliitaka ishughulikie mitaro katika maeneo ya mikocheni pembezoni mwa viwanda husika na kuondosha maji katika njia sahihi.
Kwa upande wa wenye viwanda, Mpina aliwata kuacha kutiririsha majitaka katika mazingira na kuyatibu na kuyaunga katika mfumo sahihi wa uondoshwaji maji hayo wa DAWASCO ili kunususru uharibifu wa mazingira na afya ya viumbe hai.
Aidha, Mpina aliwataka wamiliki wa kiwanda cha Bidco kuendelea kutoa ushirikiano kwa kuziba matundu yanayotoa maji machafu kutoka kiwandani hapo sambamba na kusafisha mitaro yote kiwandani humo.
 Ziara ya  siku mbili ya Naibu Waziri Mpina  jijini Dar es Salaam ilihusisha Ukaguzi wa Mazingira na Utekelezaji wa Sheria hiyo.

No comments: