Advertisements

Tuesday, October 17, 2017

MAKAMU WA RAIS AZINDUA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI MKOANI KILIMANJARO


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa  Uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yaliyofanyika katika viwanja vya Mashujaa ,Manispaa ya Moshi mjini mkoani Kilimanjaro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Mwanafunzi wa Darasa la 5 kutoka shule ya msingi Muungano Bi. Aisha Ayoub akishiriki kuima nyimbo za kuelimisha masuala ya usalama barabarani akiwa mmoja kati ya wanafunzi waliotoka shule 10 za Manispaa ya Moshi mjini wakati wa uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambao umefanyika katika viwanja vya Mashujaa ambapo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan alikuwa mgeni rasmi.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Koplo Faustina Ndunguru kutoka Makao Makuu ya Trafiki  kitengo cha Elimu ya Usalama Barabarani katika Uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yaliyofanyika katika viwanja vya Mashujaa ,Manispaa ya Moshi mjini mkoani Kilimanjaro, wengine pichani ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira (kushoto) na Kulia ni Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fortunatus Musilimu. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkuu wa Usalama na Mazingira kutoka TANROADS Makao Makuu Bi. Zafarani Madayi wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho yanayotoa elimu ya usalama barabarani katika Uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yaliyofanyika katika viwanja vya Mashujaa ,Manispaa ya Moshi mjini mkoani Kilimanjaro.
 Mkurugenzi Msaidizi Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Joyce Mbunju akimuelezea  Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan namna Wizara ilivyojipanga nakuja na mbinu za teknolojia ya kisasa katika kuhakikisha usalama barabarani unakuwepo wakati wote.

No comments: