Advertisements

Monday, December 18, 2017

AJALI YAUA WATANO NA KUJERUHI 13 MWANZA

Watu watano wamefariki dunia na 13 wajeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea katika barabara ya Mwanza kwenda Shinyanga eneo la mtaa wa Buhongwa Nyamagana mkoa wa Mwanza baada ya gari yenye namba za usajili T.107 BKK Toyota coaster kugongana na Lori

Gari hiyo aina ya Coaster ilikuwa ikiiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Badru Habibu (33) mkazi wa Nyegezi na chanzo cha ajali hiyo kimefahamika kuwa ni mwendokasi wa dereva wa Coaster aliyekuwa akijaribu kuyapita magari ya mbele bila tahadhari na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi 13.

Marehemu waliofariki katika ajali hiyo hadi sasa ametambulika jina moja tu ambaye ni 1. Abdul Mustafa, anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 42 hadi 45, huku marehemu wengine wa nne majina yao bado hayajafahamika. 


Aidha majeruhi wote kumi na tatu wapo hospitali ya rufaa ya Bugando wakipatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri, miili ya marehemu pia imehifadhiwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishina wa polisi, Ahmed Msangi anatoa wito kwa waendeshaji wa vyombo vya moto hususani madereva wa magari ya abiria akiwataka kuwa makini pindi wawapo barabarani huku wakijua wamebeba roho za watu, hivyo wazingatie sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani ili kuepusha vifo na majeruhi ya aina kama hii yanavyoweza kuepukika.

No comments: