Advertisements

Tuesday, December 26, 2017

WAUAJI WATUPA MWILI WA DEREZA WATOKOMEA NA BAJAJ

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Edward
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe. PICHA YA MAKTABA

By Burhani Yakub,Mwananchi

Tanga. Matukio ya utekaji na uporaji katika jiji la Tanga,yanazidi kuwapa hofu wananchi baada ya dereva mmoja wa bajaji,Fadhil Abubakar (20) kukutwa amekufa kwa kunyongwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni abiria waliokuwa wamemkodi.

Akizungumza leo Jumapili Desemba 24, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe amesema mauaji hayo yametokea usiku wa kuamkia jana katika eneo la Kona Z kata ya Kiomoni Tarafa ya Chumbageni.

Watu waliozungumza na gazeti hili kuhusiana na mauaji hayo, wamesema walianza kukusanyika katika eneo la Kona Z baada ya kupata taarifa kutoka kwa askari wa jeshi la Wananchi JWTZ kikosi cha Pande waliokuwa wakikimbia mchakamchaka alfajiri ya kuamkia juzi.

“Askari waliokuwa katika mchakamchaka asubuhi walipofika eneo la Kona Z wakaona mwili wa mtu aliyekufa ndipo wakatoa taarifa na sisi tukakusanyika kushuhudia”amesema Said Jumaa mkazi wa Kona Z.

Kamanda Bukombe amesema Fadhili alikodiwa na abiria juzi usiku waliotaka kupelekwa kijiji cha Pande na baada ya hapo hakuonekana tena.

“Alikodiwa na abiria walioomba kupelekwa kijiji cha Pande na walipofika Kona Z wakamnyonga kwa kamba ya katani kisha wakampora bajaji aliyokuwa akiendesha na kumtupa kwenye kichaka kilichopo kando ya barabara,” amesema Bukombe.

Amesema kituo alichokuwa akiwasubira abiria amerehemu kipo barabara ya 10 karibu na hoteli ya Asad na kwamba aliondoka saa 3.00 usiku na kupitia nyumbani kwa kaka yake barabara ya saba ambako alimuaga kuwa anakwenda nyumbani kwake Magomeni kulala.

“Baada ya hapo hakuonekana tena hadi askari wa JWTZ walipouona mwili wake ukiwa umetupwa kwenye kichaka kando ya barabara ya Amboni-Pande”amesema na kubainisha kwamba Polisi linawasaka waliohusika na mauaji hayo.
          

No comments: