Advertisements

Thursday, January 18, 2018

MAADHIMISHO YA SIKU YA POSTA AFRIKA LEO TAREHE 18 JANUARI, MWENYEKITI WA BODI YA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC), DK. HARUN KONDO ATOA SALAMU ZAKE

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, wakati alipokuwa akitoa salamu zake katika kuadhimisha Siku ya Posta Afrika, Januari 18, 2018. Kushoto ni Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe.(Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya viongozi wa vitengo vya Shirika la Posta wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Dk. Haruni Kondo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, wakati akitoa salamu zake katika kuadhimisha Siku ya Posta Afrika Januari 18, 2018.

Baadhi ya viongozi wa wafanyakazi na wa vitengo vya Shirika la Posta wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Dk. Haruni Kondo, jijini, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, wakati akitoa salamu zake katika kuaadhimisha Siku ya Posta Afrika kesho.
Baadhi ya viongozi wa wafanyakazi na wa vitengo vya Shirika la Posta wakiwa katika mkutano huo jijini.
Baadhi ya viongozi wa wafanyakazi na wa vitengo vya Shirika la Posta wakisikiliza, salamu zilizokuwa zikitolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Dk. Haruni Kondo, mbele ya waandishi wa habari, katika kuaadhimisha Siku ya Posta Afrika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya viongozi wa wafanyakazi na wa vitengo vya Shirika la Posta wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Dk. Haruni Kondo.
Baadhi ya viongozi wa wafanyakazi na wa vitengo vya Shirika la Posta wakifuatilia mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo akitoa salamu zake katika za maadhimisho ya Siku ya Posta Afrika, mbele ya waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha TPC, Elia Madulesi (kulia) na Meneja Msaidizi wa Huduma za Barua, Jasson Kalile, wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa mbele ya waandishi wa habari katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo akijibu baadhi ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari, mara baada ya kutoa salamu zake za maadhimisho ya Siku ya Posta Afrika.
Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe, akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano huo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo.
Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe, akijibu maswali ya waandishi wa habari katika mkutano huo.

Baadhi ya viongozi wa wafanyakazi na wa vitengo vya Shirika la Posta wakifuatilia mkutano huo.

Leo tarehe 18/01/2018, Shirika letu la Posta litaungana na Mashirika mengine Afrika kuadhimisha kuanzishwa kwa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) mnamo mwaka 1980.

Umoja huu makao makuu yake yapo Arusha Tanzania. Lengo la kuanzishwa Umoja huu ni kusimamia maendeleo ya Posta Afrika.

Pamoja na salaam zangu kwa Katibu Mkuu wa Umoja huu Bwana Younouss Djibrine na watendaji wenzake, napenda kuwapongeza wanaposherehekea miaka 38 ya Umoja huu.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “POSTA: Muundombinu muafaka kwa Serikali katika kufikia Malengo yake ya Maendeleo”.

Kutokana na Posta kuwa na matawi mengi yaliyosambaa katika nchi kuliko watoa huduma wengine hapa nchini, tunapongeza kauli mbiu hii na kwa kweli Shirika limejipanga katika kuhudumia wananchi katika kuwezesha mafanikio yao kibiashara, kama mnavyofahamu mwaka jana 2017 Shirika letu liliibuka kidedea katika kundi la watoa huduma (Trade Facilitation) na kukabidhiwa ngao ya ushindi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Magufuli..

Shirika letu limeanza mikakati ya kufungua vituo “Huduma Express” hapa Posta Mpya Dar es salaam na vingine vitaanza Dodoma, Mwanza, Arusha, Mbeya na Zanzibar. Katika vituo hivi tunaweza kutoa huduma mbalimbali mahali pamoja “One-Stop-Centre” na hii itasaidia sana Serikali kutoa huduma zake kwa wananchi kwa urahisi zaidi. 



Hii inaenda sambamba na kauli mbiu ya mwaka huu. “POSTA kama Muundo Mbinu muafaka kwa Serikali katika kufikia malengo yake ya maendeleo”.

Pia Dk. Kondo alitumia fursa hiyo kuelezea kwa muhtasari mafanikio na changamoto mbalimbali ambazo Shirika lilikabiliana nazo mwaka jana 2017.

Alielezea kuwa Shirika kwa ujumla lilipata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuzindua nembo mpya mwezi Desemba 2017 na sasa liko kwenye maandalizi ya kuboresha muonekano wa Shirika katika ofisi zake nchini kote.

Nawatakia Heri ya Mwaka Mpya wenye fanaka 2018.

Lt. Col. Mstaafu. Dr. Haruni Kondo

MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA

No comments: