Advertisements

Tuesday, January 2, 2018

UVCCM YAPONGEZA MIRADI YA AFYA TABORA.

Na Mwandishi wetu,Tabora

Umoja wa Vijana wa CCM umesema umeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotokana na ahadi katika ilani ya uchaguzi katika halmshauri za wilaya mji wa Nzega na Nzega vijijini mkoani Tabora.

Pia Umoja huo umeeleza kikubwa kasi hiyo inatokana na kuwepo kwa mashirikiano makubwa kati ya viongozi wa chama,halmashauri za wilaya na serikali kuu.

Matamshi hayo yametamkwa jana na Mwenyekiti wa Taifa wa UVCCM Kheri Denise james mara baada ya kumaliza kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya cha Kazogolo katika halmashauri ya mji wa Nzege .

Kheri alisema kitendo cha serikali ya awamu ya tano kupeleka jumla ya shilingi milioni mia tano toka serikali kuu oktoba mwaka huu kwa ajali ya ujenzi wa kituo hicho ni kielelezo kuwa serikali inajali maisha ya wetu wake .

"UVCCM tumeridhishwa na ujenzi wa miradi ya afya katika halmashauri za mji wa Nzega na halmashauri ya nzega vijijini.Ilani ya uchaguzi ya chama imetekelezwa kwa vitendo. Hii ndiyo tafsiri halisi ya hapa kazi "Alisems Kheir .

Aidha alisema kazi ya kuwatumikia wananchi haina mjadala badala yake inamhitaji kila kiongozi dhamana kuwa nafasi yake kuwajibika na kuwatumikia wananchi.

"Kuimarika kwa huduma za jamii na watu kupata huduma bora ndiyo malengo ya kisera yanayotakiwa kufanikishwa. Tuna wajibu kila mmoja kwa nafasi yake kumsaidia Rais na serikali yale "Alisisitiza

Kheri akiwa mkoani Tabora ametembelea mradi mkubwa wa usambazaji maji toka
ziwa Victoria mkoani mwanza kupitia shinyanga hadi Tabora,kuona maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya kazogolo na kuzumgumza na wananchi katika halmashsuri ya mji wa nzega na nzega vijiijini. 
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipokelewa na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi Nzega- mkoa wa Tabora akiwa anaelekea Mwanza kwa ajili ya mapokezi yake baada ya kuchaguliwa na mkutano mkuu wa 9 wa UVCCM kuwa mwenyekiti mpya wa UVCCM 2017-2022. 
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James wa tatu toka Kushoto akivikwa Skafu mara baada ya kuwasili katika Ofisi za CCM Wilayani Nzega.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akikagua kikundi cha ngoma mara baada ya kupokelewa.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akisaini Kitabu cha Mauzulio ya Wageni.
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Bi Tabia Maulid Mwita Akizungum,za na Wanachama wa Chaa cha Mapinduzi Wilayani Nzenga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akizungumza na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi na Jumuiya zake Wilayani nzega mkoa wa Tabora.
Wanachama Wilayani Nzega Wakimsikiliza
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice Jameswa tatu toka kushoto akizungumza jambo na M..mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya shillingi billioni 600 utakaotokea Ziwa Victoria na kunufaisha wananchi wapatao milioni 1.1 wa mikoa ya Shinyanga (vijiji 39) na zaidi Tabora (vijiji 89).
Baadhi ya Vifaa vya Ujenzi wa mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya shillingi billioni 600 utakaotokea Ziwa Victoria na kunufaisha wananchi wapatao milioni 1.1 wa mikoa ya Shinyanga (vijiji 39) na zaidi Tabora (vijiji 89).
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akitunza fedha katika kikundi cha ngoma ya Asili alipowasili Wilaya ya Nzega Vijijini kuzungumza na Viongozi mbali mbali wa chama.
Viongozi wamsikiliza
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipata maelezo toka kwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda na Mkuu wa wilaya ya Nzega Ndugu Godfrey William Ngupula,alipotembelea kituo cha afya cha Zogolo kilichopo Halmashauri ya mji wa Nzega kinachotegemewa zaidi kuhudumia wananchi wa mji wa Nzega yenye watu wasiopungua laki mmoja. Ujenzi unaolenga kuboresha utoaji wa huduma katika kituo hiki ulikadiriwa kugharimu shillingi milioni 500 ukiwa ni ufadhili wa mfuko wa World Bank.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipokelewa na Wanachama wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Shinyanga akitokea Tabora kuelekea mwanza.(Picha Zote na Fahadi SIRAJI)

No comments: