Advertisements

Monday, May 7, 2018

AWESO CUP 2018 YAZINDULIWA KWA KISHINDO, SIMBA WAILIZA YANGA PANGANI


Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza akizindua mashindano ya Kombe la Aweso (AWESO CUP 2018) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iyopita mjini Pangani, Tanga. Pembeni ni Mbunge wa Pangani na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso (mwenye kofia nyeusi) ambaye ndiye mwaandaaji wa kombe hilo, Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Mohamed Kiganja (mwenye traki suti bluu), Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza na msemaji wa Simba, Haji Manara na Jerry Muro.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza na Mbunge wa Pangani na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso (mwenye kofia nyeusi) pamoja na viongozi wengine wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Mohamed Kiganja mara baada ya kumaliza kuzindua mashindano ya Kombe la Aweso (AWESO CUP 2018) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iyopita mjini Pangani, Tanga.
Picha ya pamoja.
Wachezaji wa Simba tawi la Pangani wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi.
Wachezaji wa Yanga tawi la Pangani wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi.
Wachezaji wa Yanga tawi la Pangani wakiwapasha.
Wachezaji wa Simba tawi la Pangani wakiwapasha.
Wasanii wanaunda kundi la Uzalendo Kwanza wakifuatilia mtanange huo.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza akisalimiana na waamuzi wa mtangane. Akisalimiana na wachezaji wa Simba tawi la Pangani.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza akisalimiana nawachezaji wa Yanga.
 Tambo za watani wa Jadi, Jerry Muro akitoa yake.
 Mbunge wa Pangani na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ambaye ndiye mwaandaaji wa kombe hilo akimpa sapoti Msemaji wa Simba, Haji Manara wakati akionyesha vitu vyake. Pembeni ni Mwakibinga.
Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Zainab Abdallah Issa akipatiwa hela na Msemaji wa Simba Haji Manara.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza akisalimiana na Msemaji wa Simba Haji Manara.
Wachezaji wa Simba na Yanga wakisalimiana.
Ilikuwa ni vuta ni kuvute...
Wachezaji wakionyesha umwamba. Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza na  Mbunge wa Pangani na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso (mwenye kofia nyeusi) wakifuatilia ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Aweso (AWESO CUP 2018) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iyopita mjini Pangani, Tanga. Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza akiwa na Mkuu wa wilaya wa Pangani, Zainab Abdallah Issa wakifuatilia ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Aweso (AWESO CUP 2018) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iyopita mjini Pangani, Tanga.
Asha Boko na Tausi wakionyeshana umwamba huku Msanii Nuh Mziwanda akitoa burudani.
Umatu wa watu waliohudhuria.
Mkuu wa wilaya wa Pangani, Zainab Abdallah Issa akiongea na wanachi wa Pangani wakati wa zoezi la kugawa zawadi.
mkuu wa wilaya wa Pangani, Zainab Abdallah Issa 
 Zawadi ya Jezi zikitolewa.
Wachezaji wa Yanga na Simba wakiwa wamebeba zawadi ya Maziwa ya Asas.
Picha/Habari na Cathbert Kajuna na Oscar Assenga- Pangani.

Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza amefungua mashindano ya kombe la Aweso katika uwanja Kumba wilaya Pangani na kuwataka viongozi wa halmashauri ya Pangani kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa viwanja vya kuchezea.

Katika kufanikisha ufunguzi wa kombe la Aweso wasanii wa filamu wanaunda kundi la Uzalendo Kwanza walishiriki ili kuhamasisha vijana kupenda michezo na sanaa.

Akifungua mashindano hayo Naibu Waziri Juliana Shonza akatoa agizo kwa viongozi wa halmashauri kukarabati viwanja huku mkuu wa wilaya wa Pangani, Zainab Abdallah Issa amesema kuanzisha kwa kombe la Aweso kuanarudisha ari ya michezo wilayani humo.

Kwa upande wake Mbunge wa Pangani na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ambaye ndiye mwaandaaji wa kombe hilo amesema katika mashindano hayo watapatika vijana wenye vipaji.

Nae mwenyekiti wa uzalendo kwanza Steve Mengele 'Steve Nyerere' amesema ushiriki wao unasaidia vijana kupenda michezo na sanaa.

"Tumekuja kuwaamsha vijana wenzetu ili watambue umuhimu wa kuwa Wazalendo na kujikwamua na watambue vipaji vyao, maana vijana wengi wamepoteza matumaini ya kuishi kutokana na kujiona wametengwa na jamii" amesema.

Jumla ya timu 20 zinashiriki michuano ya kombe la uweso ambapo timu shiriki zikabidhiwa vifaa vya michezo na naibu waziri wa habari utamaduni sanaa na michezo.

Katika ufunguzi wa kombe hilo uchezwa mchezo wa mashabiki Simba na Yanga ambapo timu ya Simba ikiongozwa na Msemaji Haji Manara waliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Yanga na wakapata maziwa ya Asas na fedha laki tano huku Yanga wakipata laki tatu na maziwa ya Asas. Huku zikishuhudiwa na Naibu Waziri wa Habari Michezo, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso na Mkuu wa wilaya Pangani, Zainabu Issa, Katibu Mkuu wa BMT Mohamed Kiganja.

No comments: