Advertisements

Tuesday, June 12, 2018

SPIKA NDUGAI AONGOZA WABUNGE KUUAGA MWILI WA BABA MZAZI WA MBUNGE WA MANYONI MASHARIKI LEO KATIKA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai aongoza Waheshimiwa Wabunge katika kuuaga mwili wa Ndg. Mtuka Daniel Nguluba ambaye ni Baba Mzazi wa Mbunge wa Manyoni Mashariki, Mhe. Daniel Mtuka katika tukio lililofanyika leo tarehe 12 Juni, 2018 katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wakibeba mwili wa Baba mzazi wa Mbunge wa Manyoni Mashariki, Mhe. Daniel Mtuka aliefariki juzi  tarehe 10 Juni, 2018 katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma. Mwili huo uliagwa leo katika hospital hiyo Jijini Dodoma
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akimfariji  Mbunge wa Manyoni Mashariki, Mhe. Daniel Mtuka baada ya kuondokewa na Baba yake mzazi aliefariki  juzi tarehe 10 Juni, 2018 katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge, ndugu, jamaa na marafiki waliofika katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma kabla ya kuuaga mwili wa Baba mzazi wa Mbunge wa Manyoni Mashariki, Mhe. Daniel Mtuka katika tukio lililofanyika  leo tarehe 12 Juni, 2018  katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Spika wa Bunge, Job Ndugai (wa tatu kulia mbele), katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai (kulia mbele) wakiwa pamoja na Waheshimiwa Wabunge, ndugu, jamaa na marafiki kabla ya kuuaga mwili wa Baba mzazi wa Mbunge wa Manyoni Mashariki, Mhe. Daniel Mtuka aliefariki  juzi tarehe 10 Juni, 2018 katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma. ​
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments: