Advertisements

Thursday, June 21, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU WAJIBU WA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA KUTII SHERIA ZA NCHI ILI KUKUZA DEMOKRASIA NA AMANI YA NCH

Monica L. mnanka ( 0658717262)
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU  WAJIBU WA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA KUTII SHERIA ZA NCHI ILI KUKUZA DEMOKRASIA NA AMANI YA NCHI

Nachukua fursa hii kuwaasa Viongozi wote wa Vyama vya Siasa na wanachama kutekeleza majukumu yao ya kisiasa kwa kufuata na kuzingatia Sheria na Kanuni za Vyama vya Siasa na Sheria za nchi kwa ujumla.

Kufuatia tabia iliyojitokeza ya baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini kutumia vibaya vyombo vya habari, hususani mitandao ya kijamii kufanya vitendo au kutoa kauli ambazo zinavunja sheria za nchi, ni wito wangu kwao kuacha tabia hiyo mara moja.

Ninasisitiza kuwa Viongozi wa Vyama vya Siasa wasitumie vibaya dhana ya demokrasia na uhuru wa habari, kuvunja Sheria za nchi. Ieleweke kwamba mtu yeyote anapokiuka sheria za nchi, Sheria itachukua mkondo wake bila kujali wadhifa wa mhusika katika chama cha siasa.

Rai yangu kwa Viongozi wote wa Vyama vya Siasa na wanachama wote wa vyama vya siasa nchini, ni wajibu wa kila mmoja wao kuelewa kwamba katika kutekeleza majukumu yao ya kisiasa wanapaswa kuheshimu Sheria za nchi wakati wote ili kudumisha na kukuza demokrasia ya vyama vingi nchini. Kwa kufanya hivyo pia, Viongozi hawa watalinda na kuimarisha Amani ya nchi yetu.

 
  Jaji Francis S.K. Mutungi
MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA

No comments: