Advertisements

Friday, July 20, 2018

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE ATETA NA JAJI MKUU WA TANZANIA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akizungumza na Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma alipomtembelea Ofisini kwake leo Julai 19, 2018 jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujitambulisha rasmi tangu aapishwe kuwa Mkuu wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara, Julai 14, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike (kulia) akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Hussein Kattanga alipotembelea Ofisi ya Jaji Mkuu wa Tanzania jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike wakiteta mambo mbalimbali juu ya ushirikiano wa vyombo hivyo muhimu katika kusimamia sheria na haki. Kulia ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma(kushoto) ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Hussein Kattanga.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akiagana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma baada ya mazungumzo ambapo Kamishna Jenerali wa Magereza ameahidi kutoa ushirikiano kwa Vyombo vyote vya Haki jinai ili kutimiza majukumu yake ipasvyo(Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Makao Makuu ya Jeshi la Magereza).

No comments: