Advertisements

Thursday, August 16, 2018

NAIBU WAZIRI ,SERA ,BUNGE ,KAZI ,VIJANA ,AJIRA NA WATU WENYEULEMAVU ,STELLA IKUPA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA TANO WA THTU

Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu,Stella Ikupa akitamburishwa baadhi ya viongozi walioshiriki mkutano mkuu wa tano wa Chama cha Wafanyakazi wa taasisi za elimu ya juu Tanzania (THTU) unaofanyika mjini Moshi.
Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu,Stella Ikupa akiwasili katika ukumbi wa J.K Nyerere uliopo Chuo Kikuu cha Ushirika,Moshi (MOCu) kwa ajili ya kufungua mkutano wa Tano wa chama hicho.
Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu,Stella Ikupa akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa tano wa Chama cha Wafanyakazi wa taasisi za elimu ya juu Tanzania (THTU) unaofanyika mjini Moshi.

\Baadhi ya Wajumbe wakiwa katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa taasisi za elimu ya juu Tanzania (THTU) Dkt Paul Loisulie akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
Baadhi ya wajumbe wa mkutano huo.
Mwenyekiti wa kamati ya Wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa taasisi za elimu ya juu Tanzania(THTU),Salma Fundi akizungumza katika mkutano huo.
Kaimu Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Kippi Warioba akizungumza katika mkutano huo.
Mwakilishi wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu ca Ushirika Moshi (MOCU) Dkt Gudluck Mmari akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa taasisi za elimu ya juu Tanzania (THTU) Amina Mdidi akizungumza katika mkutano huo.
Mjumbe wa kamati ya wananwake ya THTU,Sophia Nchimbi akitoa neon la shukrani katika mkutano huo.
Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu,Stella Ikupa akiwa katika picha ya pmaoja na washiriki wa mkutano huo.

NA Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

Na Dixon Busagaga,Moshi.

CHAMA cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU) kimeiomba serikali kutunga sera ya uwepo wa eneo rafiki la kulelea au kunyonyeshea watoto katika sehemu za Kazi  pamoja na kuunda chombo cha kusimamia utekelezwaji wa uwepo wa sera ya unaynyasaji wa kijinsia katika taaasisi za elimu ya juu nchini.

Mbali na ombi hilo THTU pia kimewasilisha ombo kwa serikali la kuundwa Vyombo vya kufuatilia waajiri ambao hawazingatii maagizo ya sera zinazotungwa na serikali ili kulinda haki na maslahi ya wafanyakazi  sambamba na uwepo wa muundo wa utumishi kwa wafanyakazi waendeshaji katika taasisi za umma za elimu ya juu nchini.

Hayo yalibainishwa wakati wa mkutano mkuu wa tano wa chama hicho unaofanyika kwa siku mbili katika Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) ukishirikisha zaidi ya wanawake 80 kutoka vyuo vikuu 36,vitatu vikiwa ni vya binafsi  na 33 vya serikali .

Katika risala yao kwa mgeni rasmi ,iliyosomwa na katibu wa THTU,Amina Mdidi ,wanawake hao walisema THTU imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ya kutokuwepo kwa mwongozo wa mishahara au bodi ya kusimamamia na kudhibiti malipo ya watumishi kwa vyuo binafsi.

“Changamoto nyingine zinazootukabili ni baadhi ya taasisi kutolipa nauli za likizo kwa enza wa wafanyakazi wanawake (Mume) na watoto chini ya miaka mitano na ukosefu wa vituo rafiki kwa malezi ya watoto wachanga”alisema Mdidi.

Katika hatua nyingine ,Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania kilitoa ripoti ya utafiti juu ya utekelezaji wa sera ya maendeleo ya mwananmke na jinsia ya mwaka 2000 katika taasisi za elimu ya juu Tanzania ikionyesha aslimia 80 ya taasisi hizo zilionyesha kutokuwepo kwa masuala ya jinsia katika mpango mkakati wa taasisi.

Akisooma utafiti huo ,Mwenyekiti wa kamati ya Wanawake (THTU) taifa Salma Fundi alisema asilimia 80 ya taasisi hazikuonyesha uwepo wa mafunzo kwa wanafunzi au wafanyakazi kuhusiana na masuala ya jinsia.

“Asilimia 70 ya taasisi hazina sera ya unyanyasaji wa kijinsia ambazo ni muhimu katika kupunguza ubaguzi wa kijinsia na ukatili huku asiliamia 60 ya washiriki walikuwa na mtazamo hasi juu ya sera ya jinsia kwa kuamini ni sera inayomhusu mwanamke tu”alisema Fundi.

Katika hotuba yake Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo,Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu,Stella  Ikupa alisema THTU kwa muda mfupi kimekuwa chama kinachotoa chachu ya maendeleo na amani ndani ya taasisi za elimu ya juu Tanzania.

“Ni chama ambacho kiko makini katika shughuli zake za utatuzi na hata mfumo na uwasilishaji wa hoja zake umekuwa ni wa aina ya kipekee kwa kufanya tafiti zilizochambuliwa kwa kina wa nini wanawake wanafikilia kifanyike”alisema Ikupa.

Waziri Ikupa aliyekuwa akimuwakilisha Waziri wan chi ,ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge,KAZI,Vijana ,Ajira na Wenyeulemavu ,Jenista Mhagama aliahidi kuwasilisha mapendekezo yao pamoja na changamoto walizo wasilisha  kwa serikali  kwa ajili ya kuafanyiwa kazi.

Mwisho .  

No comments: