Advertisements

Sunday, August 19, 2018

TAMASHA LA UTAMADUNI WA MSWAHILI LAFANA, WENGI WAVUTIWA NA HARUSI ZA MILA ZA PWANI

Ms Gathoni Kamau Community Outreach Specialist Education African Advisory Committee National Museum of African Art ,Smithsonian Institution, Washington, DC akifungua tamasha la utamaduni wa Mswahili lililofanyika siku ya Jumamosi Aug 18, 2018 National Museum of African Art ,Smithsonian Institution, Washington, DC na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka nchini mbalimbali wakiwemo wazawa wa Afrika mashariki. Picha na Vijimambo Blog
Hadithi mbalimbali zilisomwa ikiwemo hadithi ya Abunuasi na Bulicheka na mkewe Elizabeth, kushoto ni Um Kulthum (Dr. Evelyn Mhina) na Aunty Jasmine walipokua wakiendesha zoezi hilo la hadithi.
Anna Mwalago akitoa simulizi kupitia njia yake ya mashairi na pia alikua mmoja wa washereheshaji wa shughuli hiyo
Huu ulikua mfano wa harusi ya utamaduni wa pwani inavyofungwa ikiwashirikisha kutoka kushoto Zain Hamza kama baba wa bibi harusi, Omar akishiriki kama Shehe, Shamis akishiriki kama baba wa bwana harusi, Jumbe Hamza kama bwana harusi na Eddie Fundi kama mjomba wa bwana harusi
Mfano wa harusi ya utamaduni wa Pwani wanongeao lugha ya Kiswahili ikiendelea.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi 
Baada ya ya ndoa kufungwa , Eddie Fundi mjomba wa bwana harusi akigawa kahawa na harua.
Kutoka kushoto ni Omar, Zain, Jumbe, Shamis na Eddie wakiwa meza kuu baada ya ndoa kufungwa. 
Aisha aliyekua kama Bi harusi akiwa amebebwa na bibi yake Um Kulthum (Dr. Everlyn Mhina) wakimsubili bwana harusi aje amfunue khanga bi harusi.
Bwana harusi akiwa tayari kumfunua bi harusi ambaye amebebwa na bibi yake.
Madada na mashangazi wa bi harusi akiwemo mama yake wakifurahia kwa kucheza mduara.
Baada ya mjomba kutoa pesa hatimae bwana harusi aliweza kumfunua uso bi harusi.
Maharusi wakipata picha ya pamoja, kushoto ni Shamis aliyeshiriki kama baba wa bwana harusi na aliyesimama nyuma ni Jamylah aliyeshiriki kama shangazi wa bwana harusi.
Maharusi wanavyoonekana siku ya pili ya sherehe yao baada ya ndoa.
Wadau mbalimbali wakiwa nje kuwasubili maharusi watakapo toka njekwa sherehe za harusi.
Maharusi wakitoka njekushereheka na wadau wengine waliohudhuria tamasha hilo la utamaduni wa Kiswahili.
Wakati wa soro
Juu ya khanga ni minoti iliyotunzwa wakati bwana harusi na ndugu zake wakila soro
Maharusi wakipata zawadi
Sherehe ya harusi ikiendelea.
Piga Box (kushoto) akipata picha ya pamoja na Cleopatra Kulasi ambaye pia ni Katibu wa Jumuiya ya waTanzania DMV
Piga Box(kulia) akipata picha na Shamis Abdulah
Kushoto ni Shamis akifanyiwa mahojiano na Luninga wa sauti ya Amerika(VOA TV)
Ma Winny Casey akipata picha namwanamitindo Diana Magesa
Ma Winny Casy akipata picha na Teen Miss Tanzania USA (kilia ndiye aliykua mshindiwa shindano hilo)
Diana Magesa (kati) akiwa na teen Miss Tanzania USA
Jamylah
Kushoto ni Lysa Bantu ambaye pia ni mweka hazina wa Jumuiya ya waTanzania DMV
Sunday Shamarina Anna Mwalago wakipata picha ya pamoja ambao wote walikua washereheshaji wa tamasha.

No comments: