Advertisements

Tuesday, September 18, 2018

Irene Uwoya: “Vyovyote unavyosikia kuhusu mimi amini, Na Ikibidi Ongezea na Vingine Pia"

Muigizaji Irene Uwoya  ametumia ukurasa wake wa instagram kupost picha yake na kuandika maneno ya lugha ya kiingereza ambayo kwa haraka haraka yanahusishwa kuwa inawezekana ni kutokana na kinachoendelea kati yake na mumewe dogo janja.

Kabla ya  Uwoya kuposti huo ujumbe, Dogo Janja ndiye aliyeanza kwa kupost ujumbe tata uliowashangaza wengi.

Dogo Janja aliweke picha ya mkewe Irene Uwoya na kuandika; “BADO NA IMANI YOTE NA PITIA🙏🏻 😌”, hali iliyowafanya mashabiki waanze kuamini tetesi kwamba huenda ni kweli wameachana.
Baada ya ujumbe huo wa Dogo Janja, Irene Uwoya naye akaandika;  “Vyovyote unavyosikia kuhusu mimi amin, sina tena muda wa kujielezea mwenyewe, pia unaweza kuongezea baadhi ya vitu kama unataka”

No comments: