Advertisements

Wednesday, November 14, 2018

SPIKA WA BUNGE JOB NDUGAI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UGENI KUTOKA BENKI YA NMB OFISINI KWAKE JIJINI DODOMA

 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na ugeni kutoka Benki ya NMB ulioongozwa na Ofisa Mkuu wa Mikopo wa Benki hiyo, Ndg. Tom Borghlos (wa pili kushoto) walipomtembelea leo tarehe 14 Novemba 2018 Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Wa tatu kushoto ni Mjumbe wa Bodi, Ndg. Jos Lange, Afisa wa Benki ya NMB, Ndg. Juliana muwanga (wa tatu kulia), Mkuu wa Biashara Benki ya NMB, Ndg. Donatus Richard (wa pili kulia) na Meneja kanda ya kati, Ndg. Nsolo Mlozi

 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Ofisa Mkuu wa Mikopo wa Benki ya NMB, Ndg. Tom Borghlos (wa pili kushoto) pale ugeni kutoka Benki hiyo ulipomtembelea leo tarehe 14 Novemba 2018 Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Mjumbe wa Bodi NMB, Ndg. Jos Lange na Afisa wa Benki ya NMB, Ndg. Juliana muwanga
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka Benki ya NMB ulioongozwa na Ofisa Mkuu wa Mikopo wa Benki hiyo, Ndg. Tom Borghlos (watatu kulia) walipomtembelea leo tarehe 14 Novemba 2018 Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akiagana na Mjumbe wa Bodi wa Benki ya NMB, Ndg. Jos Lange pale ugeni kutoka Benki ya NMB ulipomtembelea leo tarehe 14 Novemba 2018 Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto ni Mkuu wa Biashara Benki ya NMB, Ndg. Donatus Richard. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments: