![]() |
Mdau wa
Michezo Dkt.Musa Mdede akiwa ameshika kombe la ushindi la timu ya Nzihi FC wakati wa tukio hilo la kuwapongeza.
|
Na Andrew Chale.
Mdau wa
Michezo na aliyekua mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga Mwaka 2015, Dkt.Musa Mdede
ameahidi kuisapoti timu ya soka ya Nzihi
mpaka kufika daraja la kwanza baada ya ubingwa wa kihistoria wa mkoa walioupata
hivi karibuni.
Ameyasema
hayo jana alipohudhuria sherehe ya kuipongeza timu ya Nzihi Fc
iliyofanyika katika Ofisi za kijiji cha Nzihi iliyopo Wilaya ya Iringa
Vijijini.
Katika
sherehe hiyo Dk.Mdede alitoa kiasi cha fedha shilingi laki moja (
100,000/-) kama zawadi kwa ushindi
walioupata vijana hao kama hamasa huku pia akiwahidi kuwasaidia kufikia malengo
yao makubwa katika michezo.
Katika mashindano ambayo Nzihi iliibuka mabingwa, yalishirikisha
jumla ya timu 22 kutoka mkoa wote wa Iringa.
"Shabaha
yetu ni kuona Nzihi Fc inafika daraja la kwanza.Tutaisapoti timu yetu kadri ya
mahitaji yake, kwani Nzihi Fc ni fahari ya Kata yetu ya Nzihi, Jimbo letu la
Kalenga na Mkoa wa Iringa kwa ujumla" Alisema Dk.Mdede.
Aidha Dk.Mdede
ameahidi kutoa vifaa mbalimbali vya michezo kama mipira,fulana za mazoezi, koni
kwa ajili ya mazoezi na vitu vingine
mbalimbali vya msaada wa timu hiyo.
Dk. Mdede
amesema vifaa hivyo anatarajia kutoa kabla ya kuanza kwa mashindano ya kanda ambayo Timu
hiyo ya Nzihi Fc itashiriki kama mwakilishi wa mkoa wa Iringa.
Aidha,
katika sherehe hiyo ilihudhuliwa na wananchi, wadau na Viongozi mbalimbali wa Serikali
akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera ambaye akuwa mgeni rasmi,
Diwani wa Kata ya Nzihi, Stephen Mhapa pamoja na viongozi wengine akiwemo
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa vijijini.
![]() |
| Mdau wa Michezo Dkt.Musa Mdede wa kwanza kushoto waliokaa akiwa pamoja na wachezaji wa Nzihi FC wakati wa tukio hilo la kuwapongeza. |
![]() |
| Mdau wa Michezo Dkt.Musa Mdede wa akizungumza katika tukio hilo juu ya kuisaidia Nzihi FC wakati wa tukio hilo la kuwapongeza jana . |



No comments:
Post a Comment