Advertisements

Tuesday, February 19, 2019

MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MKALAMA MKOANI SINGIDA

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ibaga wilaya ya Mkalama ambao waliusimamisha msafara wake kwa lengo la kumsalimu ,Makamu wa Rais yupo kwenye ziara ya kikazi mkoani Singida. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Naibu Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso akijibu hoja za wananchi wa Ibaga (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Wilaya ya Mkalama mkoani Singida. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassanakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi(wa pili kulia) wakati wa ukaguzi wa daraja la Sibiti  ambalo limekamilika kwa asilimia 94.8%.
 Muonekano wa daraja la Sibiti ambalo kwa mujibu wa taarifa za Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) walizozitoa wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassa ambapo wamesema ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 94.8%. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa daraja la Sibiti kutoka kwa Kaimu Meneja Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Singida Mhandisi Matari J. Masige (kushoto) ambalo limekamilika kwa asilimia 94.8%,kulia ni Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Naibu Waziri wa Maji Mhe. Juma Awesu akimsalimia Lailat Ramadhani mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya Sekondari ya Iguguno wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan mkoani Singida. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments: