
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, mapacha hao na mama yao Rosemary wana chembechembe za kufanana kwa asilimia 99.999.
Mapacha hao ambao wamekuwa gumzo mitandaoni katika siku za karibuni katika nchi za Afrika Mashariki baada ya picha zao kuonekana hadharani wakionyesha kutoka katika familia mbili tofauti licha ya kufanana.
Lakini jana kitendawili cha wasichana hao wanaotoka kaunti ya Kakamega kiliteguliwa ambako imebainika kwamba msichana wa tatu, Melvis Mbaya, ambaye amekuwa nao mara kwa mara si ndugu yao halisi katika kuzaliwa.
Uamuzi huo ulifikiwa Aprili mwaka huu baada ya familia hizo kuomba msaada wa vipimo vya DNA ambako taasisi ya Lancet Kenya ikajitolea kufanya kazi hiyo kwa gharama nafuu.
Kwa mujibu wa matokeo hayo, sehemu 12 kati ya sehemu 23 zinazotumika katika tathmini hiyo ya Melvis Mbaya zilikosa kufanana.
No comments:
Post a Comment