Advertisements

Saturday, October 30, 2021

WAZIRI ATOA MSAMAHA NA USALIMISHAJI WA SILAHA ZINAZOMILIKIWA KINYUME NA SHERIA

30/10/2021 DODOMA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. George Simbachawene ametoa msamaha na usalimishaji wa silaha kwa wanaomiliki kinyume na sheria na kuwataka kuzisalimisha silaha hizo kwenye vituo vya Polisi na wahusika kutoshitakiwa endapo watazisalimisha silaha hizo haramu kwa hiari na kwa muda uliopangwa.

Waziri Simbachawene ametoa msamaha huo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa zoezi la usalimishaji wa silaha haramu kwa hiari nchi nzima litafanyika kuanzia tarehe 01 Novemba 2021 na baada ya muda uliowekwa kupita, msako mkali utafanyika kwa nchi nzima ili kuwakamata wote waliokaidi nafasi ya msamaha waliopewa.

No comments: