ANGALIA LIVE NEWS

Monday, March 7, 2022

MZEE SADALLA JUMA SADALLA ALIYEMBAKA MSICHANA WA KAZI KUFIKISHWA MAHAKAMANI VUGA ,UNGUJA JUMATATU 07 Mach 2022.


Juhudi za kukomesha Ubakaji na udhalilishaji visiwani Zanzibar hatimaye
Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla mwenye umri wa miaka 74 mkazi wa Bububu,Unguja,atafikishwa mahakamani Vuga,Unguja siku ya tarehe 07 Machi 2022 kwa makosa ya kumbaka msichana wake wa kazi mwenye umri wa miaka 15 (jina limeifadhiwa). 

Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla alifikishwa mahakamani mara ya mwisho siku ya 21 Machi 2022 na mahakama ilikuwa inasikiliza mashahidi mabalimbali kwa upande wa mashataka yake na kesi hiyo imepangiwa tena tarehe 03 Machi 2022 katika mahakama ya Vuga mjini Unguja. Katika juhudi la kukomesha vitendo vya ubakaji na udhalalishaji viwani Zanzibar,serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na vyombo vya ulinzi vinajitahidi kuwafikisha mbele ya sheria wale wote watakaotenda makosa hayo ya ubakaji na udhalilishaji.

Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla alilalamikiwa na wanaharakati visisiwani Zanzibar kuwa ni mzoefu katika vitendo vya ubakaji pamoja na udhalalishaji na alipombaka msichana wake wa kazi mwenye umri wa miaka 15 ,alikuwa yupo huru na alipanga kuondoka unguja kukimbia kesi hiyo baadhi ya majirani zake walisika lakini vyombo vya usalama viliwahi kumshika na hatimaye kumpeleka mahakamani.
Mshitakiwa Sadalla Juma Sadalla yupo mahabusu kwa kuwa shitaka la kubaka,udhalalishaji halina dhamana .

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt.Hussein Ally Mwinyi imepania kukomesha vitendo vyote vya Ubakaji na udhalalishaji,pamoja na madawa ya kulevya vinakoma kabisa visiwani Zanzibar.

 

No comments: