Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akifungua kikao kazi cha ofisi yake
na Viongozi wa Vyama vya
Wafanyakazi jijini Dodoma kilichoandaliwa kwa lengo la kupata maoni ya
wadau yatakayoboresha mfumo mpya wa Usimamizi wa
Utendaji Kazi kwa watumishi wa Umma (Public
Employees Performance Management Information System-PEPMIS) ambao
utaanza kutumika rasmi kuanzia mwezi Julai, 2022.
Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi
wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi
cha ofisi yake na viongozi hao, kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la
kupata maoni ya kuboresha mfumo mpya wa usimamizi wa utendaji kazi kwa
Watumishi wa Umma.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira, Vijana na Wenye, Ulemavu
Mhe. Prof. Joyce Ndalichako na Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi wakifuatilia mada kuhusu mfumo mpya wa Usimamizi wa Utendaji Kazi kwa watumishi wa Umma utakaoanza
kutumika rasmi Serikalini kuanzia mwezi Julai, 2022.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira, Vijana na Wenye, Ulemavu Mhe. Prof. Joyce
Ndalichako akifunga kikao kazi Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Viongozi wa Vyama vya
Wafanyakazi jijini Dodoma, kilichoandaliwa kwa lengo la kupata maoni ya wadau
yatakayoboresha mfumo mpya wa Usimamizi wa
Utendaji Kazi kwa watumishi wa Umma utakaoanza kutumika rasmi Serikalini
kuanzia mwezi Julai, 2022.

No comments:
Post a Comment