Wednesday, August 7, 2024

RAIS DKT. SAMIA AZINDUA KIWANDA CHA SUKARI CHA MKULAZI MKOANI MOROGORO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akiweka Jiwe la Msingi kwenye Uzinduzi wa Kiwanda Cha Sukari Cha Mkulazi kilichopo Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro akihitimisha Ziara yake Mkoani humo leo August 07,2024.

Sehemu ya kiwanda cha Sukari Mkulazi ambapo miwa hupokelewa na kuchakatwa katika hatua za awali, ambacho kimezinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mbigiri mkoani Morogoro, tarehe 7 Agosti 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi, Watumishi na Wananchi wa maeneo Jirani mara baada ya kuzindua kiwanda cha Sukari Mkulazi, Mbigiri mkoani Morogoro, tarehe 7 Agosti, 2024.


No comments: