Saturday, August 17, 2024

RAIS WA ZANZIBAR AJUMUIKA NA WANANCHI KATIKA SALA YA MAZISHI MSIKITI WA KWABOBO KIDONGOCHEKUNDU ZANZIBAR


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj .Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Familia na Waumini wa Dini ya Kiislam katika Sala ya Maiti, ya marehemu Sheikh Yussuf Mohammed aliyekuwa Imamu Mkuu wa Msikiti wa Kwaboko Wilaya ya Mjini Unguja, ikiongozwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi,iliyofanyika 16-8-2024 baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa katika msikiti huo, (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Idrissa Kitwana Mustafa na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Sheria,Katiba,Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Mhe.Haroun Ali Suleiman .(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj .Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Familia na Waumini wa Dini ya Kiislam katika kuitikia dua ya kumuombea marehemu Sheikh Yussuf Mohammed aliyekuwa Imamu Mkuu wa Msikiti wa Kwaboko Wilaya ya Mjini Unguja, ikisomwa na Sheikh Abdallah Talib,baada ya kumalizika kwa Sala ya Maiti,iliyofanyika 16-8-2024 baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika msikiti huo.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk,.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kutowa mkono wa pole kwa Mtoto wa Marehemu Sheikh Yussuf Mohammed aliyekuwa Imamu Mkuu wa Msikiti wa Kwaboko Wilaya ya Mjini Unguja Ndg.Shaali Yussuf Mohamed,baada ya kumalizika kwa Sala ya Maiti na Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti wa Kwaboko 16-8-2024.(Picha na Ikulu)

No comments: