Friday, October 11, 2024

TPA KUANZA USIMAMIZI WA MWALO WA KIRUMBA WILAYANI ILEMELA

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) inatarajia kuanza rasmi usimamizi wa shughuli zote za kibandari katika mwalo wa Kirumba ulipo Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza kufuatia tangazo lililotolewa kwenye gazeti la Serikali.

Akitoa taarifa kwa umma Ijumaa Oktoba 11, 2024 kupitia waandishi wa habari, Meneja Bandari Kanda ya Ziwa Victoria, Erasto Lugenge alisema hatua hiyo ni utekelezaji wa tangazo la Serikali namba 855 la tarehe 24/12/2023 ambalo linaipa TPA mamlaka ya kusimamia mialo yote iliyo rasmi.

Lugenge aliongeza kuwa shughuli za usimamizi wa mwalo huo zitaanza kesho rasmi Jumamosi Oktoba 12, 2024 zikihusisha usimamizi wa usalama wa vyombo vya majini.

Awali mwalo huo ulikuwa ukisimamiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ukiwa ni miongoni mwa mialo 10 katika Ziwa Victoria iliyotangazwa kusimamiwa na TPA.
Na George Binagi- GB Pazzo, Mwanza
Meneja Bandari Kanda ya Ziwa Victoria, Erasto Lugenge akitoa taarifa kwa umma kuhusu TPA kuanza kuusimamia mwalo wa Kirumba wilayani Ilemela.
Meneja Bandari Kanda ya Ziwa Victoria, Erasto Lugenge akizungumza na wanahabari jijini Mwanza.
Tazama Video hapa chini

No comments: