Wednesday, December 5, 2012

MAJONZI MAKUBWA: AJALI MBAYA IRINGA, YAUWA WATU 6 WA FAMILIA MOJA WAFARIKI KATIKA AJALI IRINGA WAKIELEKEA MBEYA. SHUHUDIA

Gari lililopata ajali la Rav 4 T 770 BNP eneo la Tanzangozi, Iringa lililokua likiendeshwa na Bw. Ezekiel Mwaiteleke(Marehemu) majira ya saa sita na nusu mchana na kusababisha vifo vya watu watano wa familia moja papo hapo December 4, 2012



Baadhi ya kina mama wasamaria wema wa Tanzangozi Iringa wakijaribu kumpepelea mmoja ya majeruhi wa ajali iliyotokea December 4, 2012 huko Tanangozi, Iringa likihusisha Toyota Rav 4 T 770 BMP lililoingia nyuma ya Trailer T 566 BNQ ambapo watu watano wa familia moja waliokua wakitokea Dar kwenda Mbeya walifariki papo hapo
Gari aina ya Scania lenye cabin # T 840 BST likiwa na Trailer # T 566 BNQ likiwa limegongwa kwa nyuma na Toyota Rav 4 T 770 BNP huko Tanangozi, Iringa na kusababisha vifo vya watu watano wa familia moja papo hapo
Wasamaria wema wakitoa moja ya maiti kutoka katika gari Toyota Rav 4 T 770 BMP huko Tanangozi, Iringa
Ajali mbaya imetokea mkoani Iringa mchana wa leo na kusababisha vifo vya watu wanne wa familia moja pamoja na mfanyakazi wa ndani mmoja.


Ajali hiyo imetokea katika eneo la Tanangozi wilaya ya Iringa kwenye kizuizi cha barabara cha mafundi wa kutengeneza barabara kuu ya Iringa -Mafinga mkoani Iringa mida ya saa nane mchana
Kwa mujibu wa mashuda wa tukio hilo wameueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari dogo aina ya Rav 4 lenye namba za usajili T 770 BMP kulipalamia lori lenye tela kwa nyuma. 

Huku chanzo kikitajwa kuwa ni kuendesha kwa mwendo kasi wa dereva wa gari ndogo marehemu Ezekiel Mwaiteleke na kushindwa kulimudu na kulipalamia lori kwa nyuma.

Kwa mujibu wa mashuda wa tukio hilo wameueleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari dogo aina ya Rav 4 kuendesha kwa mwendo kasi na kushindwa kulimudu na kulipalamia lori kwa nyuma na kuwa gari hiyo ilikuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Kyela mkoani Mbeya.

Hivyo katika ajali hiyo abiria wote wanne akiwemo baba na mama wa watoto wawili waliokuwemo katika gari hiyo pamoja na watoto hao kufa papo hapo na maiti zote kupelekwa katika Hospitali ya mkoa wa Iringa.

Majina ya waliokufa ni pamoja na Ezekiel Mwaiteleke ambaye ni dereva wa gari hilo na baba wa familia hiyo ,mkewe Grace Mwaiteleke ,mtoto Kelvin Mwaiteleke (2),Happy Mwandike na mfanyakazi wao wa ndani aliyefahamika kwa jina la Linda Ezekiel huku majeruhi katika ajali hiyo ni mmoja na amekimbizwa Hospital ya mkoa wa Iringa.

FRANCISGODWIN.BLOGSPOT.COM

No comments: