Email address:ccmwashdc@gmail.com
TANGAZO LA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA CCM TAWI LA DMV
Wanachama wa CCM DMV mnaombwa kuhudhuria mkutano mkuu wa kuchagua viongozi wa CCM katika Tawi La DMV utakaofanyika:
SIKU: JUMAMOSI March 16, 2013
MUDA: SAA 9 JIONI (3pm) Tafadhali zingatia muda.
MAHALI: 500 Sligo Avenue
Silver Spring,Md 20910
Ili uweze kupiga kura hakikisha una kadi yako ya Chama na uwe mwanachama hai, na kama huna kadi au umepoteza tafadhali wasiliana na Katibu wa Tawi Ndugu
Faraja Isingo, Simu ( 301-592-7581)
Nafasi zitakazogombaniwa ni :
1) Mwenyekiti wa tawi
2) Katibu wa Tawi
3) Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa Tawi
4) Katibu wa Fedha na Uchumi wa tawi
5) Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Tawi (UVCCM)
6) Katibu wa Umoja wa Vijana wa Tawi (UVCCM)
7) Mwenyekiti Umoja wa Wanawake (UWT)
8) Katibu wa Umoja wa Wanawake ya Tawi (UWT)
9) Mwenyekiti Umoja wa Wazazi wa Tawi
10) Katibu wa Umoja wa Wazazi ya Tawi
11) Wajumbe 10 wa halmashauri ya Tawi
SIFA ZA MGOMBEA:
1. Awe na umri kuanzia miaka 18
2. Umri kwa nafasi za Umoja wa Vijana(UVCCM)ni kuanzia miaka 16-30
3. Awe mwanachama hai wa CCM mwenye kadi
4. Mtanzania mwenye pasipoti ya nchi nyingine pia anaweza kugombea
5. Mtanzania ambaye hawezi kutoka nje ya Marekani pia anaweza kugombea.
KAMA UNA SWALI LOLOTE KUHUSU UCHAGUZI TAFADHALI WASILIANA NA TUME YA UCHAGUZI:
1.Hidaya Mahita(240)-271-7799(Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi)
2.Zainab Buzohela(202)-403-9732
3.Anton Mkai(240)-643-0267
4.Baraka Daudi(301)-792-8562
No comments:
Post a Comment