Tuesday, March 26, 2013

UMOJA WA MATAIFA WAKUMBUKA UTUMWA NA BIASHARA YA UTUMWA

BANGO lililombeba ujumba wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kumbukumbu ya utumwa na biashara ya utumwa, maadhimisho ambayo yalifikie kilele Marchi 25 hapa Umoja wa Mataifa.

Professa Ali Mazrui, Mwanazuoni maarufu akisaidiwa kuketi kabla ya kuzungumza katika siku hii ya maadhimisho ya kumbukumbu ya utumwa na biashara ya utumwa 

Professa Mazrui akizungumza ambapo pamoja na mambo mengine alielezea histotia ya utumwa na biashara ya utumwa pamoja na harakati mbalimbali zilizopelekea kukomeshwa kwa biashara hiyo. pamoja na kusisitiza haja na umuhimu wa kuendelea kuwaenzi waathirika wa ukatili huo, alitaka pia kuenzi yale mema ambayo baadhi yake ni matokeo ya historia hiyo ya Utumwa, Professa Mazrui alikuwa mzungumzaji mkuu katika maadhimisho haya ambayo hufanyika Machi 25 ya kila mwaka.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, ambapo pamoja na mambo mengine alisisitiza Jumuiya ya Kimataifa kuendelea kupambana na utumwa unaoendelea hivi sasa kila pembe ya dunia.
hii ni Nakala Halisi ya Tangazo la Ukombozi wa Watumwa ( Emancipation Proclamation) iliyotiwa sahihi mwaka 1864 na Rais Abraham Lincoln na aliyekuwa Waziri wake wa Mambo ya Nje wakati huo, Bw. William H. Seward. Nakala hii ambayo ilioneshwa pamoja na maonesho mengine yaliyohusu utumwa na biashara ya utumwa ni kati ya nakala 48 ambazo Rais Lincoln alizisaini, na zikauzwa kwa dola kumi kila moja kati ya juni 7 hadi 29, 1864 huko Philadelphia kwa lengo la kupata fedha za kuwasaidia maveterani wa vita. inasemekana ni kati ya nakala hizo 48 ni 26 tu ndiyo bado zipo moja ikiwa ni hii ambayo ilipatikana kwa hisani ya Bw. Lawrance

Na Mwandishi Maalum
Mwanazuoni Maarufu Professa Ali Mazrui, amesema,  wakati jumuiya ya kimataifa  inapokumbuka, ukatili, ubaguzi, unyanyasaji na kila aina ya uovu aliotendewa mtu mweusi kupitia utumwa na biashara ya utumwa,  yapo mambo mazuri ambayo kwayo anasema yapashwa kuenziwa.

Alikuwa akizungumza wakati wa  siku ya Kimataifa ya  kumbukumbu ya  Utumwa na Biashara ya Utumwa, ambayo imeadhimishwa jana ( jumatatu ) hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Mwanazuoni huyu maarufu na  mtaalamu aliyebobea katika Historia ya Bara la Afrika na anayeheshika sana, alikuwa mzungumzaji mkuu katika siku hii ambayo miaka sita iliyopita,  Baraza Kuu la Umoja wa mataifa  liliitenga rasmi Machi 25 ya kila mwaka kama siku  maalum ya  kuwakumbuka na kuwaenzi waathirika wa  ukatili huu uliofanyika zaidi  ya miaka 400 iliyopita.

“ Leo hii tunapowaenzi na kuwakumbuka wahanga wa utumwa na biashara ya utumwa,  na historia nzima ya harakati zilizopelekea  kukomeshwa kwa biashara hii, lazima pia tujifunze  kutoka na histollia ile  kwa   kutambua na kuenzi mema ambayo baadhi yake yanatokana na  historia hiyo.” akasema  Professa Mazrui.
Kwa habari na picha zaidi bofya read more
Kwa  mtizamo wake, anayataja  baadhi ya mambo hayo kuwa ni pamoja urithi ulioachwa na Martin Luther King ( jr), mambo mazuri yaliyofanywa na  Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini Mzee Nelson Mandela, Marekani kuwa na Rais wa kwanza mwenye asili ya Afrika,  Katisa Katoliki kuwa na Papa wa  Kwanza kutoka Amerika ya Latini, wanawake kuendesha  harakati za  kujiwezesha  na kujikomboa kiuchumi na kuibuka kwa mataifa mapya  yanayokua kiuchumi duniani.


 Professa Mazrui ambaye alionekana wazi kuelemewa na utu uzima, licha ya kuelezea kwa kina harakati mbalimbali zilizochangia kwa namna moja ama nyingine  kukomeshwa  kwa  utumwa na biashara ya utumwa, alitumia fursa ya siku hii, kumkumbuka na kumuenzi Chinua Achebe aliyefariki wiki iliyopita. Professa akamuelezea  Chinua Achebe kama mmoja ya watu mahiri na mashuhuri ambaye kwa kutumia kalamu yake alipigania utu, heshima , hadhi na utamaduni mwa mtu mweusi. Akasema dunia na hasa  Afrika imempoteza mtu muhimu sana.

Awali akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, aliitaka Jumuia ya Kimataifa  kuelekeza nguvu zake katika kuukabili utumwa na biashara mpya ya utumwa inayoendelea kushika kasi hivi  katika kila pembe ya dunia.

Akautaja utumwa huo kuwa ni pamoja na  biashara ya utumwa wa ngono, ajira za watoto wadogo,  biashara ya usafirishaji wa binadamu na   matumizi ya watoto wadogo katika vita.
Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya kumbukumbu ya  utumwa na biashara ya utumwa  yalitanguliwa na shughuli mbalimbali zilizofanyika kwa wiki zima.

Baadhi ya shughuli hizo  zilikuwa ni pamoja na mijadala ya kisomi iliyowashirikisha watafiti na wataalamu wa historia ya utumwa na  ukomeshaji wake,  mijadala iliyowashirikisha wanafunzi kutoka mabara mbalimbali,  mijadala ya Asasi zisizo za Kiraia na maonesho ya muziki na    Nakala Halisi   ya  Tamko la Ukombozi wa Watumwa, nakala hii ni kati ya  nakala chake zisizozidi 48 ambazo   Rais Abraham Lincoln na Waziri wake wa Mambo ya Nje Bw. William H. Seward walitia sahihi mwaka 1864.Benson
Steel Pulse mwanamuziki wa kimataifa wa muziki wa Rock ambaye amekuwa akitumia kipaji chake kuelimisha na kuhamasisha kuhusu ukatili anaotendewa mtu mweusi, Bw. Steel Pulse alikuwa kati ya wanamuziki waliotumbuiza katika tamasha maalum la kuwaenzi waathirika wa utumwa na biashara ya utumwa.
Omi Mwanamziki wa Kizadi kipya wa Muziki wa Jazi, kutoka Afrika ya Mashariki naye aliwapagaisha washiriki wa tamasha la muziki kwa vibao vyake murua vilivyokuwa na radha ya muziki wa Jazi kwa kuchanganya na midundo ya kibantu ambayo mwenyewe anaita " New African Jazz" Somi alitambuliwa kama Baba yake ni Muganda na Mama yake Mnyarwanda
Kikundi cha Utamduni kutoka nchini Cameroon wakitumbuiza wakati wa Tamasha maalum la Muziki kuadhimisha kumbukumbu ya waathirika wa utumwa

hawa pia wanatoka Cameroon wakiburudisha

Biashara ya utumwa haikufanyika kupitia bahari ya Atlantik peke yake bali hata Bahari ya Hindi kwa watumwa waliotoka Afrika ya Mashariki, Balozi za Tanzania na Kenya katika Umoja wa Mataifa, zilifanya onesho la Khanga zilizobeba ujumbe mbalimbali, kama sehemu ya kuenzi utamaduni mwa mwafrika na wakati huo huo kukitangaza kiswahili, washiriki wa tamasha la utamaduni ambalo lilikukwenda samabamba na vyakula vya asili ya afrika walifurahia sana tafsri ya kila ujumbe uliokuwa katika khanga hizo.
wanamuziki hawa waliokuwa pamoja na Steel Pulse wakicharaza magitaa yao kwa uhodari mkubwa pali kuwa hapatoshi
  Wanamuziki hawa walisindikiza mwanamziki mwigine kutoka Afrika ya Magharibi, Benyoro ambay naye alikuwa kivutio kikubwa
Benyoro akifanya vitu vyake
Mwanamuzi mwingine maarufu kwa kulicharaza gitaa na ambaye pia ni Mjumbe Maalum wa UNESCO katika mradi wa kutafiti njia za Biashara ya Utumwa akiimbia kwa hisia kali wakati wa Tamasha la Muziki, Marcus Miller amewahi kushinda mara mbili Tuzo ya Grammy katika midundo ya American Jazz

No comments: