Saturday, January 9, 2016

Hafla Mchapalo ya Tigo na Wanamitandao ya Jamii

Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Mtandao wa Thehabari.com, Joachim Mushi akitoa neno la shukrani kwa Kampuni ya Tigo kwa kuwakutanisha baadhi ya wamiliki na waendeshaji wa mitandao ya kijamii (bloggers & website owner) katika hafla hiyo maalumu ya chakula cha jioni iliyofanyika 'Double Tree hotel' jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa ambao ni wamiliki wa mitandao ya kijamii (bloggers & website owner) wakiwa katika hafla maalumu ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na kampuni ya Simu ya Tigo kusherehekea mteja wa milioni moja katika 'Facebook' ya kampuni hiyo. Tigo ilitoa zawadi mbalimbali kwa wateja wanaofuatilia ukurasa wao (Facebook page).
Msanii maarufu wa dansi nchini, Christian Bella akiwaburudisha wageni waalikwa katika hafla maalumu ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na kampuni ya Simu ya Tigo kusherehekea mteja wa milioni moja katika ukurasa wa 'Facebook' wa kampuni hiyo.
Msanii maarufu wa dansi nchini, Christian Bella (kulia) wa Bandi ya Malaika kulia akicheza na mmoja wa wageni waalikwa katika hafla maalumu ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na kampuni ya Simu ya Tigo kusherehekea mteja wa milioni moja katika 'Facebook' ya kampuni hiyo.
Baadhi ya wanamitandao ya jamii wakisakata rumba na msanii maarufu wa dansi nchini, Christian Bella (wa tatu kulia) toka Bandi ya Malaika alipokuwa akiwaburudisha wageni waalikwa ambao ni wamiliki wa mitandao ya kijamii (bloggers & website owner) katika hafla hiyo maalumu ya chakula cha jioni iliyofanyika 'Double Tree hotel' jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanamitandao ya jamii wakisakata rumba na msanii maarufu wa dansi nchini, Christian Bella (wa pili kulia) wa Bandi ya Malaika alipokuwa akiwaburudisha wageni waalikwa ambao ni wamiliki wa mitandao ya kijamii (bloggers & website owner) katika hafla hiyo maalumu ya chakula cha jioni iliyofanyika 'Double Tree hotel' jijini Dar es Salaam.
"...TWANGA PHOTOOO..." Baadhi ya wanamitandao ya jamii wakiji-selfie na Msanii maarufu wa dansi nchini, Christian Bella wa Bandi ya Malaika mara baada ya kutoa burudani.
Mshereheshaji wa hafla hiyo, Taji Liundi (kulia) akimkaribisha Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Mtandao wa Thehabari.com, Joachim Mushi kutoa neno la shukrani kwa Kampuni ya Tigo kwa kuwakutanisha baadhi ya wamiliki na waendeshaji wa mitandao ya kijamii (bloggers & website owner).
Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Mtandao wa Thehabari.com, Joachim Mushi (kushoto) akibadilishana mawazo na mmoja wa maofisa kutoka kampuni ya Tigo, Shavkat Berdiev katika hafla hiyo.

No comments: