Advertisements

Thursday, May 17, 2018

Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza atembelea JNIA

 Koplo Chesco Mbise akimwongoza mbwa anayeitwa Max-Z kuondoka mara baada ya zoezi la kuonesha namna anavyokamata dawa za kulevyia katika mizigo ya abiria kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), ambapo leo Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza (hayupo pichani) alipotembelea na kuona zoezi hilo. Mbwa huyu ni kati ya wawili waliotolewa kwa msaada na serikali ya Marekani.
Askari Hadson Muhuma akiwa amemshika mbwa anayeitwa Nopi wakati akifanya zoezi la kutambua mizigo ya abiria yenye nyara za serikali zikiwemo pembe za Ndovu, lililofanyika leo kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), baada ya kutembelewa na Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza (hayupo pichani).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (mwenye suti ya bluu kulia), leo akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza, Bw. Matthew Rycroft mara baada ya kukamilika kwa zoezi la mbwa wa polisi kuonesha namna wanavyokamata dawa za kulevyia na nyara za serikali katika mizigo ya abiria kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha (kulia) akiongea na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela baada ya zoezi la mbwa kuonesha namna wanavyobaini mizigo yenye nyara za serikali na dawa za kulevyia leo kiwanjani hapo.
Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza, Bw. Matthew Rycroft (wapili kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (wa pili kulia) wakimsikiliza Bw. Matt Jenkins (aliyekaa), ambaye ni Afisa wa UK Border Force wa Kitengo cha dawa za kulevyia katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). (Picha zote na Bahati Mollel wa TAA). 

No comments: