Advertisements

Thursday, April 18, 2019

MTANDAO WA WANAWAKE WA AFRIKA WANAOJISHUGHULISHA NA UVUVI ‘AWFISHNET’ WAKUTANA DAR, WAFANYA MKUTANO MKUU WA MWAKA


 Katibu Mkuu wa AWFISHNET, Bi. Editrudith Lukanga  akizungumza kwenye mkutano huo wa kwanza uliofanyika leo Aprili 18,2019, Jijini Dar es Salaam.



MTANDAO wa Wanawake wa Afrika wanaojihusisha na shughuli za uvuvi, uchakataji wa samaki na mazao yake (African  Women Fish Processors and Traders Network- AWFISHET)  kutoka nchi 28 za Afrika wamekutana Jijini Dar es Salaam katika mkutano Mkuu wa kwanza  wa mwaka kujadiliana namna ya kutatua changamoto za masoko na namna ya kuendeleza shughuli zao.

Awali akifungua mkutano huo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina uliofunguliwa kwa niaba yake na Bi. Flora Luhanga kutoka wizara hiyo  aliwataka Wanawake wa Afrika kuwa kitu kimoja haswa katika utungaji wa sera zenye kuwajenga na zenye kuwaweka kwenye njia sahihi za maendeleo.

Waziri Mpina aliwataka wanawake hao kuwa kioo kwa wengine pindi watakaporejea kwenye nchi zao  kwani anahakika mijadala na mambo mbalimbali waliojifunza kwenye mkutano huo ni ishara tosha kuwa kwa sasa wanafikia malengo yao kama wanawake katika sekta ya uvuvi Bara la Afrika.

Nae Rais wa AWFISHNET, Bi. Beyeue Ateba Baliaba amewataka Wanawake hao kuendelea kuwa kitu kimoja na kuleta kwa pamoja mawazo yao ili yaweze kutatuliwa kwa sauti moja.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa AWFISHNET, Bi. Editrudith Lukanga  amewataka Wanawake wa Afrika kushiriki kikamilifu kwani mkutamo huo utajadili mkakati wa nmna ya kushughulikia changamoto  kwenye nchi zao  na namna ya kuzitatua.

“Mkutano huu wa siku mbili, unashirikisha wajumbe zaidi ya 60, kutoka nchi 28 za Bara la Afrika hasa Wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi.

Leo kila mjumbe amewasilisha mada na namna ya shughuli anazofanya nchini mwake ili kuona tunafikia malengo yetu kwa pamoja ikiwemo namna ya kutafuta na kupata mitaji, masoko, miundombinu ya uchakataji na mambo mengine yanayofanana na hayo.” Alisema Bi. Editrudith Lukanga.

Bi. Editrudith Lukanga  aliongeza kuwa, mkutano huo, wajumbe wataweza kushiriki katika maasuala mbalimbali yakiwemo utengenezaji sera, sheria, kanuni pamoja na utekelezaji wake kama msingi mkubwa wa kuwezesha sekta kuwa endelevu na pia kuchangia kwenye lishe na usalama wa chakula.
Aidha, amewashukuru wadau waliowezesha mkutano huo wa mwaka na wa kwanza kwa mafanikio makubwa huku akiendelea kuwaomba waendelee kuwasapoti zaidi.

“Mwanamke ni kiungo cha jamii, kwani ukimsapoti mwanamke, umesapoti jamii nzima katika kupambana na  umasikini. Uwepo wetu hapa umewezeshwa na sie pamoja na wadau wetu. Natoa wito kwa Serikali zote  wanakotoka Wanachama wetu waweze kuweka mikakati  ya makusudi ya kuwatambua kazi zao na kuweza kuwasaidia.

AWFISHNET imeanzishwa mnamo Aprili 17, 2017 huku ikiwa na wajumbe kwenye jumuiya za Kitaifa za wanawake wanajishughulisha na uvvuvi katika nchi zao. Katika mkutano huo wajumbe washiriki zaidi ya 60,  Nchi za Afrika ikiwemo Tanzania, Zambia, Uganda, Tunisia, Togo, Tanzania, Sudani Kusini, Sierra Leone, Senegal, Nigeria, Mauritania, Mali, Malawi, Madagascar, Liberia, Kenya.

Pia wapo kutoka: Guinea, Ghana, Misri, DR. Congo,  Ivori cost, Congo, Comoro, Chad, Cameroon, Burundi, Burkina Faso, Benin na  Algeria.


Baadhi ya Wajumbe wakiwa kwenye mkutano huo

Makamu wa Rais wa AWFISHNET, Bi.Jeriedayaro Uwhraka akizungumza kwenye tukio hilo 

Mwakilishi Shirika la Chakula Duniani (FAO)  kwa Afrika, Martin Van Der Knaap akizungumza kwenye mkutano huo wakati wa ufunguzi


Bi. Flora Luhanga akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina.


 Katibu Mkuu wa AWFISHNET, Bi. Editrudith Lukanga  akizungumza kwenye mkutano huo wa kwanza uliofanyika leo Aprili 18,2019, Jijini Dar es Salaam. 





No comments: