Advertisements

Friday, November 26, 2021

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWATEMBELEA WACHEZAJI WA TEMBO HEROES

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akizungumza na wachezaji wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa watu wenye ulemavu (Tembo Heroes) wakati alipowatembelea leo katika uwanja wa Mkapa na kuwapa salamu za Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kuelekea katika mashindano ya kufuzu kushiriki kombe la Dunia.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuzungumza na wachezaji wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa watu wenye ulemavu (Tembo Heroes) wakati alipewatembelea leo katika uwanja wa Mkapa na kuwapa salamu za Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kuelekea katika mashindano ya kufuzu kushiriki kombe la Dunia.
Mlezi wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa watu wenye ulemavu(Tembo Heroes), Mh. Riziki Lulida akitoa neno la shukrani kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Wakati Waziri Mkuu alipowatembelea wachezaji hao katika uwanja wa Mkapa na kuwapa salamu za Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kuelekea katika mashindano ya kufuzu kushiriki kombe la Dunia kwa watu wenye ulemavu.
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa watu wenye ulemavu (Tembo Heroes) wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa (hayupo pichani) wakati alipewatembelea leo katika uwanja wa Mkapa na kuwapa salamu za Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kuelekea katika mashindano ya kufuzu kushiriki kombe la Dunia.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Wachezaji wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa watu wenye ulemavu (Tembo Heroes) wakati alipewatembelea leo katika uwanja wa Mkapa na kuwapa salamu za Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kuelekea katika mashindano ya kufuzu kushiriki kombe la Dunia.

Picha na WUSM – Dar es Salaam

No comments: