Friday, January 19, 2024

DIWANI SAME MJINI ATAKA WANAFUNZI SHULENI WAPEWE CHAKULA BORA, MILO MITATU

 

Na Ashrack Miraji Same kilimanjaro

DIWANI wa Kata ya Same Mjini mkoani Kilimanjaro Mritha Emezitaka Shule ambazo zipo kwenye kata yake kuhakikisha zinapika chakula Bora Kwa wanafunzi wanaosoma shule hizo

Mritha ameyasema hayo akiwa katika  ziara za kukagua miradi mbalimbali ndani ya Kata yake ambapo alitembelea Shule ya Msingi N.A  iliyopo Wilaya ya Same mkoani kilimanjaro kukagua idadi ya wanafunzi waliofika  shuleni na ubora wa chakula kinachoandaliwa shuleni kwa ajiri ya wanafunzi

"Nikutoe rai kwa wazazi  wenzangu wenye watoto kwenye shule yoyote iliyopo katika Kata yoyote kuhakikisha watoto wao wanakula mashuleni kwani nijukumu la mzazi kuhakikisha mwanae anapata milo mitatu kwa siku kwa mujibu wa sheria, "amesema

Ameongeza kuwa "Kuna baraka ya kipekee sana kwa mzazi hata kwenye shuhuli zako za mihangaiko mwanao anapokuwa amekula na kushiba tena kwa jasho lako.Ikumbwe kwa mzazi kufanya jukumu lake hilo litaleta chachu kwenye matokeo ya watoto wetu."

Pia  Diwan Mritha amesema wao  Madiwani wanajukumu  zito la kumsaidia Rais Dk.Samia Suluhu Hassani kwa Kazi kubwa anayoifanya Katika kuleta Maendeleo kwenye Taifa  ni Mama ambaye anajua uchungu wa watoto wetu .

Akizungumzia kuhusu yaliyofanywa na Rais Dk.Samia wilayani Same , amesema Rais Samia ameyafanya mambo makubwa yakiwemo ya ujenzi wa shule nyingi ndani ya Wilaya hiyo.

"Tunamshukuru Rais Samia kwa kutuletea fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo, amefanya mambo makubwa kwa kushirikiana na Mbunge wetu wa Jimbo la Same Magharibi David Mathayo ambaye amekuwa akipambana kuhakikisha jimbo letu linakuwa na maendeleo."

Amewaomba wananchi wa Same kuendelee kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassani pamoja na Mbunge wao kwani wamekuwa wakifanya kazi kubwa na nzuri ya kuhakikisha maendeleo yanapatikana.


 

No comments: