Advertisements

Thursday, April 25, 2024

PSPTB YAWAFIKIA WANACHUO WA CHUO CHA BAHARI DAR ES SALAAM



Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee akitoa maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo wakati wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa Astashada, Stashada na Shahada wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kilichopo jijini Dar es Salaam.

Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetoa mafunzo Wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) hii ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu kwa umma hasa kwenye vyuo vinavyotoa masomo ya Ununuzi na Ugavi.
Akizungumza na Michuzi Blog, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee amesema Bodi hiyo imeendelea kuwapa mafunzo Wanafunzi wa Vyuo mbalimbali wanaochukua kozi hiyo ya Ununuzi na Ugavi kuhusu shughuli zinazofanywa na Bodi, Usajili kwa njia ya mtandao pamoja na maadili na miiko ya taaluma hiyo.

Naye, Kaimu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Jonnes Lugoye ametoa shukrani kwa wafanyakazi wa PSPTB kwa kuweza kufika chuoni hapo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Bodi.
Kaimu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi - DMI, Jonnes Lugoye akiwakaribisha wageni kutoka Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) walipofoka Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu Bodi hiyo.
Afisa Ununuzi kutoka Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB),  Ally Yassin Mbarouk akitoa maelezo kuhusu namna ya kuongeza dhamani kwenye taaluma hiyo kwa wanafunzi wa Astashada, Stashada na Shahada wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kilichopo jijini Dar es Salaam.

Afisa TEHAMA Mwandamizi kutoka PSPTB Elihuruma Eliufoo akitoa mada kuhusu namna ya mwanafunzi anavyoweza kujisajili kwenye mfumo wa Bodi (ORS) pamoja na kufanya mitihani ya Bodi wakati wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa Astashada, Stashada na Shahada wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kilichopo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wa Astashada, Stashada na Shahada wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) wakiuliza maswali kwa wafanyakazi wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) aliofika chuoni hapo kwa ajili ya kutoa elimu .
Baadhi ya wanafunzi wa Astashada, Stashada na Shahada wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) wakifuatilia mada kutoka kwa wafanyakazi wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) waliofika chuoni hapo kwa akili ya kutoa elimu zinayohusu Bodi hiyo.
Kaimu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi - DMI, Jonnes Lugoye akiwakabidi wanafunzi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) walioshinda zawadi akati wa mafunzo yaliyotolewa na Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) 
 Kaimu Mkuu wa Idara ya Sayansi na Menejimenti - DMI, Elinathan Blasius akitoa neno la shukrani kwa wafanyakazi wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) waliofika chuoni hapo kwa akili ya kutoa elimu zinayohusu Bodi hiyo.


Picha za Pamoja

No comments: