Advertisements

Tuesday, April 16, 2024

TCAA YAPONGEZWA USIMAMIZI THABITI SEKTA YA USAFIRI WA ANGA



Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bw. Daniel Malanga akiwasilisha majukumu ya Mamlaka mbele ya Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar lipotembelea Makao Makuu ya TCAA kujionea na kujifunza shughuli za usimamizi wa sekta ya usafiri wa anga nchini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar Yahya Rashid Abdallah akizungumza mara baada ya kamati hiyo kupata taarifa ya kazi zinazofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
Baadhi ya wanakamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar  wakiuliza maswali mara baada ya kupata maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) walipotembelea makao makuu wa Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanakamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar, Watumishi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, watendaji wa Mamalaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA), Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakifuatilia mada iliyokuwa inatolewa kuhusu Mamlaka hiyo. 
Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) Godlove Longole akitoa ufafanuzi kuhusu mafunzo yanayotolewa katika chuo hicho kwa Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar waliofika chuoni hapo kwa ajili ya kujifunza na kujua kazi hasa za TCAA
Picha ya pamoja


Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar imesifu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kwa jitihada inayofanya katika usimamizi wa sekta ya usafiri wa anga Tanzania bara na Zanzibar na kupelekea kuimarika usalama wa usafiri wa anga nchini.

Wajumbe wa kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Mhe. Yahya Rashid Abdallah wametoa pongezi hizo wakati walipotembelea Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakiongozana na watendaji wa Mamalaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA) kwa ajili ya kujifunza na kuongeza uwezo wa kusimamia anga kwa njia za kisasa zenye usalama zaidi.

Akiupokea ujumbe huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Daniel Malanga amesema hata sasa wakati taifa linatimiza miaka 60 ya muungano, Mamlaka itaendelea kusimamia sekta hii muhimu kwa kufuata misingi na miongozo yote stahiki ya kitaifa na kimataifa ili Taifa liendelee kuvutia wawekezaji wengi zaidi katika sekta hii adhimu.

Wajumbe wa Baraza wamesema usalama wa anga unatakiwa kupewa kipaumbele na kutazamwa kwa upana wake katika kuimarisha huduma za uongozaji ndege ili kuiwezesha anga kuwa salama na kuleta tija.

Aidha wajumbe hao wameisisitiza TCAA kuhakikisha wakati wote inakua mstari wa mbele katika kupokea teknolojia mpya za sekta ya anga ili kuhakikisha taifa haliachwi nyuma na mageuzi yanayotokea kwa kasi duniani.

Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya baraza la wawakilishi ipo Tanzania bara kwa ajili ya shughuli za kawaida za kamati hiyo.

No comments: