Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu amefanya mazungumzo ya faragha na rais Barack Obama wa Marekani katika ikulu ya White House.
Ni mazungumzo yao ya kwanza tangu serikali za nchi hizo mbili kutofautiana hadharani hivi karibuni, kuhusu mpango wa Israeli wa ujenzi wa makazi mapya ya wayahudi mashariki mwa Jerusalem.
Wakati wa ziara yake nchini Marekani Bwana Netanyahu amerejelea kile alichosema ni haki ya Israeli ya kujenga mjini Jerusalem.
''Jerusalem ni mji mkuu wa Israeli na si makazi'', alieleza Bwana Netanyahu.
No comments:
Post a Comment