ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, May 30, 2010

MSAKO WA PIKIPIKI MORO


Na Dunstan Shekidele,Morogoro,
KUTOKANA ogezeko la ajali za pikipiki kutokea kila mara Mkoani Mrogoro jeshi la polisi mkoani hapa limeendesha msako mkali na kukamata waendesha pikipiki hizo bila kuwa na leseni.

Mwandishi wetu alifika katika kituo kikuu cha usalama barabarani mkoa wa morogoro na kukuta lundo la pikipiki zikiwa zimekamatwa kwa makosa mbali mbali ikiwemo kosala la kuendesha bila leseni.

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa morogoro[RTO] lbrahim Mwamakula alipohojiwa na mwandishi wetu kuhusiana na opresheni hiyo,alisema kwamba zoezi hilo limeanza juzi na kwamba zaidi ya pikipiki 82 zimekamatwa kwa makosa mbali mbali.

"Safari hii hatuta kuwa na huruma na mtu, juzi na jana tumeshakamata pikipiki zaidi ya 82 unazoziona hapo nje,na kwamba leo tumefanikiwa kuwapeleka mahakamni madereva 8 kwa kosa la kuendesha pikipiki bila ya kuwa na leseni na hawa ndio wanaosababsiha ajali nyingi,. alisema

Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya morogoro,Bw Thabiti Said Mwambugu ameitisha semina ya madereva wote wa pikipiki wa wilaya ya morogoro mjini ndani ya ukumbi wa Bwalo la umwema

No comments: