ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, May 30, 2010

Wakazi wa Magomeni; Walalamikia Bonde la Mkwajuni,Magomeni


Na Andrew Chale


WAKAZI wa Magomeni na Mkwajuni Manispaa ya Kinondoni wamelitaka jeshi la Polisi kuimalisha Ulinzi katika bonde la Mkwajuni,kufuatia vibaka kupola na kujeruhi wananchi nyakati za usiku.
Wakizungunza na.......... jana kwa nyakati tofauti jana jijini Dar esa Salaam wakazi hao, walidai kuwa  wanakabiliwa na wakati mgumu kutoka kwa vijana wa kihuni ambao wanakaba wapiti njia majira ya jioni na kuwanyang’anya mali pamoja na kujeruhi.
Mengi ya madai hayo wakazi hao walidai kuwa Diwani wa Kata ya Magomeni Julian Bujugo   alidai kuwa ameshindwa kuondoa kero za wanchi ambao wanakabiliwa na usalama mdogo.
“Diwani wa Kata ya Magomeni, ameshindwa kutatua tatizo ili kwa muda mrefu sasa, msitu huu umekuwa ukipoteza maisha ya watu na mali zao kila siku lakini yeye ameshindwa kuingilia kati’ walisema wakazi hao walipokuwa wakionghea na........
Wakazi hao waliendelea kudai kuwa, licha ya kulipoti kero zao hizo, katika vyombo vya usalama lakini hamna hata maamuzi sahihi yaliyochukuliwa huku kil siku wakishambuliwa na vibaka wanao jificha kwenye poli hilo.
“Tumelallamika juu ya swala ili kwa muda mrefu sasa juu ya kuondolewa huu msitu, upunguzwe ama utolewe kabisa lakini hamna hatua zilizochukuliwa” walidai.
Uchunguzi uliofanywa na ...... ili kwa siku kadhaa, uliweza kubaini matukio mbalimbali ya kihalifu wanaofanyiwa wapitanjia, yakiwemo ya kupolwa mali mali zao na kudhuriwa.
Huku idadi kubwa ya wanaopolwa katika bonde hilo ni wapanda baiskeri wanaokatisha majira ya alfajiri ya asubuhi na jioni, ambapo wahalifu hao inadaiwa wanakaa katika poli hilo na pindi wanapofanywa uhalifu huo wanakimbilia humo.
“Wapanda baiskeri mara kwa mara wanapolwa, tunaomba wasiwe wanajiamini kukatisha katika bonde hili majira ya jioni ni hatari kwao pamoja na wapita njia” kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo alipotafutwa Diwani wa Kata hiyo ,Bujugo akuweza kupatikana kulizungumzia swala hilo.

No comments: