ANGALIA LIVE NEWS

Monday, June 14, 2010

Kilele cha Uchangiaji wa Damu Dar es Salaam, Biafra leo Juni 14




 Wananchi waomba kuchangi bila woga
Na Andrew Chale
WANANCHI wa jijini  wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangia  mpango wa damu salama ilikuokoa na kuzuia vifo kwa akinamama wajawazito ,watoto na wahanga wa ajali.
 Hayo  yalisemwa jana na Meneja wa mpango wa damu salama Kanda ya Mashariki, Grace Mlingi alipokua akiongea na waandishi wa habari juu ya maadhimisho ya uchangiaji wa damu salama ambayo kitaita inafanyika jijini Mwanza kwene Viwanja vya Gand.
“Tunawaomba wananchi waendelee kuchangia damu bila kuogopa ilikuokoa wananchi wote wanaoitaji damu pindi wapatapo matatizo yakiwemo ya pindi akinamama wanaojifungua, ajali na watoto” alisema.
Aliendelea na kusema kuwa, mpaka sasa kunaitajika uniti nyingi za damu ilikukizi mahitaji ya nchi. “ Nchi inaitaji Uniti za damu salama lita  laki tatu na nusu,lakini hazitoshi, hivyo malengo yetu ni kuhakikisha tunakusanya lita 100 kwa siku.”
Kwa upande wake Afisa viwango kanda ya mashariki, Ndeunasia Towo alisema kuwa wataendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kuchangia damu ilikukidhi mahiti kwa walengwa.
“Mpaka sasa tunaendelea kuamasisha klabu za wachangia damu ambazo nyingi zimeundwa mashuleni na nyingine ni za watu binafsi” alisema Towo.
Katika uchangiaji huo ambao ulianza tokea Juni Mosi tayari wamesha kusanya damu lita 300, huku wakiendelea kuwaamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kuchangia.
Aidha, inadaiwa kuwa katika kilele cha maazimisho hayo ya uchangiaji wa damu salama, kwa nchi zilizoendelea  siku ya kilele huwa ni siku ya kuamasisha na kubadilishana mawazo lakini kwa nchini hali ni tofauti kufuatia watu wengi kukosa muhamko wa kuchangia.
“Mpango wa kuamasisha uchangiaji huu nchini ulianza  tokea mwaka 2004 ambapo mwaka 2005 zilianzishwa Kanda maalum za damu na kufikia kanda nane kwa nchi nzima.” Hayo yalibainishwa na Towo ambaye ni  Afisa viwango Kanda ya Mashariki inayounganisha mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Dodoma .
Katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Biafra , shule mbalimbali za Sekondari pamoja na watu binafsi walijitokeza na kuchangi damu hiyo.
“Tunaomba Serikali itunge michakato sahihi juu ya uchangiaji wa damu mashuleni, kwani miaka ya nyuma watu walikuwa wanamwamko wa kuchangia lakini kwa sasa kutokana na matatizo pamoaja na magonjwa watu wengi wameogopa kuchangia damu” alisema Kharim Jumbe ambaye ni mwanafunzi wa Makongo.
Wananchi wengi wanaogopa kuchangia damu hivyo wameondolewa hofu na kujitokeza kwani damu hiyo wanaochangi anaenda kuwasaidia watanzania wote.Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘wachangiaji vijana damu pya dunia ya leo’

No comments: