ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, December 13, 2011

WIMBO WA KUNDI LA TANZANIA GOSPEL ALL STARS WAPATA HESHIMA YA KUWA WIMBO MAALUM KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU ‏

Wimbo wa kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Tanzania ulioimbwa na Tanzania Gospel All stars (Waimbaji nyota wa muziki wa 
injili Tanzania), umepata hadhi na heshima ya kuwa wimbo maalumu katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara.
Chini ya mwalimu John shabani na usimamizi wa chama cha muziki wa injili Tanzania(Chamuita), Waimbaji hao walipewa nafasi maalum ya kuimba wimbo huo mbele ya Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete na mbele ya marais wa nchi mbalimbali, mawaziri, wabunge, mabalozi,  pomoja na maelfu ya watu waliohudhuria katika maadhimisho hayo.
Viongozi na watu mbalimbali wamewapongeza waimbaji hao wa injili kwa umoja na mshikamano wao, pia wameupongeza wimbo huo, hivyo kuwaomba kuusambaza wimbo huo kwa watanzania ili kila mtu abarikiwe na wimbo huo
Hii ni mara ya kwanza kwa waimbaji wa injili kuungana pamoja na kurekodi wimbo wa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya uhuru wa Tanzania.
Video ya wimbo huo inategemea kusambazwa kwa watanzania kwa gharama ndogo.
Waimbaji walioshiriki kurekodi wimbo huo ni:
1. Gloria kilahiro                                            18. Mzee Makassy

2. Amon Kilahiro                                            19. Mzungu Four

3. Masanja Mkandamizaji                                20  Jane Misso

4. Upendo kilahiro                                            21 Addo November

5. Stella Joel                                                  22. Mheshimiwa Martha Mlata

6. Nely Nyamanga                                         23. Ambwene mwasongwe

7. Joyce Ombeni                                                                                                                    

8.  Bony Mwaitege                                          24. Douglas Pius

9. John Shabani                                              25. Mchumu Maximillian

10. Rose Manoza                                              26. Charles Thobias Malya

11. Yona Abiud                                                  27. Joshua makondeko

12. Miriam Lukindo Mauki                                  28. Daniel Safari

13. Robert Bukelebe                                          29. Naomy Mbwambo

14. Nicholaus Misuzi                                          30. Joseph kasigala

15. Christina Matai                                             31. Debora Said

 16. Tina Marego                                               32. Stara Thomas  

17. Martha Mwaipaja                                        33. Victor Ahron

Na wengine wengi.
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania

Picha kwa hisani GPL

1 comment:

Anonymous said...

Hongera sana Waimbaji wa Kiinjili kwa kumtukuza Mungu katika sherehe za miaka hamsini ya Uhuru. Mungu Awabiriki Nyote.