ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, November 14, 2012

salamu za pongezi


Tawi la DMV
P.O.BOX 56356 WASHINGTON DC 20040
 Email address:ccmwashdc@gmail.com

13th November, 2012

PONGEZI KWA VIONGOZI WAPYA WA CCM TAIFA


Chama Chama Mapinduzi hapa Marekani kinatoa pongezi kwa viongozi wapya waliochaguliwa katika mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma. Kwa niaba ya wana CCM hapa Marekani tunatoa pongezi za dhati:
MWENYEKITI WA CCM TAIFA
Mheshimiwa, Dr. jakaya Mrisho Kikwete
MAKAMU MWENYEKITI CCM TAIFA- TAZANIA BARA
Mheshimiwa, Philip Mangula
MAKAMU MWENYEKIT CCM TAIFA- ZANZIBAR
Mheshimiwa, Dr. Mohamed Sheni
Mheshimiwa, Jakaya Mrisho kikwete anaendelea kuleta misingi imara ya uongozi bora, uadilifu, ukweli, ubunifu wa sera na usimamizi imara wa utekelezaji wa sera na itaki za chama. Kama mwenyekiti aliyepita ameweza kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi katika serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Juhudi za kudumisha amani, umoja na kukemea rushwa ndani ya chama. Na kufanikiwa kujumuisha wanachama wa rika mbali mbali na kuweza kushirikiana pamoja katika kuboresha chama.
Mheshimiwa, Phili Mangula anaendelea kutumikia chama akiongeza upeo wake wa siasa na itikadi, Uongozi wa dhati na ubunifu wa siasa mpya katika mfumo huu wa vyama vingi. Mheshimiwa mangula anaongeza uzoefu wake wa siasa na itikadi.
Mheshimiwa, Dr. Mohamedi Sheni, akiongeza ubora na ujuzi wa uadilifu na umakini katika maamuzi.

Kwa niaba ya wanachama wote wa CCm washio nchini Marekani tunawapongeza viongozi hawa wa ngazi ya taifa katika kipindi kijacho.
Viongozi wote waliochaguliwa wa NEC Tanzania bara na Zanzibar
Viongozi hawa watasaidia uwezo wao katika kukiimarisha chama.
Shukurani zimwendee, Mheshimiwa Jakaya Mrisho kikwete katika mipango ya mataarisho mazuri ya mkutano mkuu. Wanachama wote wa CCM tumefarijika kuona mkutano huu unafanyika kwa njia ya utulivu, amani, umoja, haki na upendo. Vile vile, tukitathimini utendaji wa chama katika kipindi kilichopita tumefarijika kuona chama kimejengeka katika misingi imara. Kubwa zaidi, wanachama wote wa chama cha mapinduzi ndani na nje ya Tanzania tumefarijika katika hatua ya serikali ya kupanga mipango madhubuti, kusimamia utekelezaji wake na kufikia mafanikio ya kukabiliana na changamoto mbali mbali za maendeleo ya jamii ya wananchi na uchumi wa nchi.
Haya ni baadhi ya mafanikio ya chama cha mapinduzi katika kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa kupitia serikali ya jamhuri wa muungano wa Tanzania.
HALI YA UCHUMI
Katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi serikali inaendelea kubabiliana na changamoto mbali mbali za maendeleo ya uchumi wa Tanzania. Serikali iliweza kuweza kupanga mipango na usimamizi imara juu ya mipango wa kufungua fursa kwa ukuaji uchumi, ujenzi wa mazingira ya maendeleo ya viwanda na uimarishaji ubunifu uchumi ambao umeweza kukua kwa asiliamia 7 mwaka 2012. Takwimu hizi zinaonyesha namna gani jinsi uchumi wa Tanzania unavyokua kwa kasi kama nchi za India na China. Vile vile, hali hii inaonyesha kuwa mbali na changamoto za upandaji wa bei ya gesi na matatizo ya kiuchumi ya nchi za bara la Ulaya na Marekani lakini serikali imeweza kutafuta mbinu na mipango ya kukuza uchumi kwa wastani wa 6% mpaka 7% kwa mwaka. Kwa kweli lengo la serikali la ukuaji uchumi kwa 12% kwa mwaka na kuweza kuinua hali ya maisha ya mtanzani linatia moyo. Hatua nyingine ambayo serikali imeweza kufanikiwa ni kuongezeka kwa soko la uuzaji wa bidhaa za Tanzania nchi za nje, hali hii imeweza kufungua mwanya wa biashara ndogo ndogo kwa wananchi. Takwimu zinaonyesha Tanzania imeweza kuongeza Export kutoka dola za kimarekani 2,945.5 mwaka hadi kufikia dola za kimarekani 7,461.2 mwaka huu. Serikali imeweza kuongeza akiba ya fedha za kigeni katika benki kuu kufikia dola za kimarekani 4.1, hali hii inaihakikishia moja kufikia kiwango cha kimataifa na kuiwezesha nchi kuweza kuagiza biadha kutoka nje kwa muda takribani miezi 4. (3.8). Jingine ni Jinsi serikali ilivyoweza kuchukua hatua za kukabiliana na upunguzaji wa mlipuko wa bei (inflation) kutoka 19.8% na kufikia 13.5% mwaka huu. Hii ina maana inasaidia kupunguza ukali wa maisha kwa mwananchi. Lakini, bado tunaimani jitihada zinafanya hili kupunguza mpaka single digit  (chini ya asilimia 10%) hasa katika vyakula.
MAPATO YA SERIKALI
Serikali ya awamu ya nne imeweza kuongeza mapato ya serikali kutoka TSH. trilion 4.13 mwaka 2005/2006 mpaka kufikia TSH. trilion 8.8.  Kama tunavyojua bajeti ya serikali ni TSH. trilion 15.2. Vile vile, hali hii inaoshesha namna gani serikali ilivyoweza kupunguza kutegemea misaada katika bajeti kutoka 44% mpaka 21%. Juhudi nyingine zilizoleta mafanikio ni upangaji uzuri wa matumizi ya serikali katika bajeti ya mwaka 2012/2013 ambayo itato kipaombele za kiipa elimu 24%, miundo mbinu 16% na afya 10% ya bajeti yote. Kwa kweli juhudi hizi ni za kuungwa mkono kwani nchi nyingi duniani zimeweza kupiga hatua katika maendelea ya jamii na uchumi kwa kwa kuweza kuweka fungu kubwa katika sekta hizo. Serikali, imeweza kupata mafanikio katika kukagua matumizi mbali mbali ya mashirika na wizara za serikali kwa kutumia ofisi ya mkaguzi mkuu wa taasisi za serikali. Hatua hii imeweza kuwafichua wale wafanyakaji wa umma ambao wanafuja fedha za serikali.
UWEKEZAJI
Serikali ya awamu ya nne, katika kutekeleza ilani yake ya uchaguzi imeweza kuweka mipango na usimamizi imara wa miradi ya gesi, viwanda, kilimo, madini na huduma ya fedha. Takwima za serikali zinaonyesha katika mwaka 2011 kumekuwepo na miradi 826 yenye thamani ya dola za kimarekani 7,177 na itakayoweza kutoa ajira 79,00 kwa wananchi wa Tanzania katika kipindi kijacho.
MIUNDOMBINU
Juhudi nyingine za serikali ya awamu ya nne ni ile kutoa kipau mbele katika uboreshwaji wa miundombinu ardhini, majini na angani. Bajeti ya serikali ni asilimia 16%. Nchi inapoweza kuboresha miundombinu inaweza kusaidia kupunguza gharama za usafiri, uimarishaji wa shughuli za viwandani, kutoa mwanya ya biashara kwa wananchi wa mji mmoja na mji mwingine. vile vile, jitihada hizi zinaweza kusaidia kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi na kuwapatia wananchi kipato katika mwanya wa kuongeza uzalishaji wa taifa. Takwimu zinaonyesha mpaka sasa serikali inafanya jitihada za ujenzi wa  barabara za lami na za kisasa zenye urefu wa  kilometa 11,154 zinaenda kukamilika. Kwa kweli hatua hii ya serikali inastahili kuungwa mkono kwa Tanzania na nchi ambayo inajiimarisha kwa kuwa na bara bara bora ukilinganishwa na nchi za jirani. Mwisho, serikali imeweza kudhiirisha uwezo mkubwa wa ujenzi kwa kutumia fedha za serikali badala ya kutegemea fedha za wafadhili kutoka nje kwa 60% gharama zote za ujenzi na mfuko wa fedha za barabara ( Roads fund).

ELIMU
Serikali ya awamu ya nne imeweza kutenga 24% ya bajeti yote ya serikali katika sekta ya elimu. Hii ni hatua nyingine muhimu ukilinganishwa na nchi nyingine katika bara la Afrika. Hatua hii imeweza kuongeza idadi kubwa kwa watoto wenye umri wa kuingia elimu ya msingi na kutoa huduma hii bure bila gharama. Takwimu za serikali zinaonyesha Tanzania ni nchi pekee inayoongoza kwa asilimia 97% barani afrika kuwa na idadi kubwa ya uandikishaji na upatikanajia wa elimu ya awali. Kwa kweli utekelezaji huu unatia moyo kwa sababu kiwango ambacho kimewekwa na agizo la malengo ya milenia yaliyowekwa na umoja wa Taifa in 100% itakapofika 2015. Serikali imeweza kujenga shule za sekondari  3,165 kutoka mwaka 2005 mpaka sasa. Hatua hii ya serikali ikishirikiana na sekta binafsi na wananchi wa kata imeweza kutoa fursa ya wanafunzi wengi kuendelea na elimu ya sekondari. Mfano, idadi ya vijana wanaojiunga na shule za sekondari imeongezeka kutoka wanafunzi 524,325 mwaka 2005 mpaka 1,884,272 mwaka huu. Sasa hivi Tanzania ina idadi ya vyuo vikuu 27 nchini. Vile vile, jitihada hii imeweza kutoa mwanya kwa wanafunzi kuendelea na elimu ya juu. Takwimu za serikali zinaonyesha kuwa idadi imeweza kuongezeka kutoka wanafunzi 40,719 na kufikia 166,482 hadi sasa. Serikali imeweza kupanua huduma ya utoaji wa mikopo kwa wanafunzi ambao hawawezi kumudu gharama za elimu ya juu. Serikali ya awamu ya nne imeweza kuongeza fedha kwa ajili ya mikopo kutoka TSH bilion 56.1 mwaka 2005 mpaka TSH bilion 306. Kisha, idadi ya wanafunzi wanaonufaika na huduma hii imeweza kuongezeka kutoka 16,345 mpaka wanafunzi 93,176 mwaka huu. Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma ambacho kinajengwa na fedha za serikali. Ujenzi wa chuo hichi utaweza kuchukua wanafunzi 40,000. Tunaamini, serikali bado inafanya jitihada katika kuboresha kiwango cha elimu kinachotolewa nchi. Serikali inaimarisha sera na viwango vya elimu ili kuweza kupima kiwango cha ubora wa elimu ya wanafunzi. kutoa elimu ambayo italingana na makakwa ya muajiri.  Ujenzi wa nyuma za walimu hasa hasa vijijini, uimarishaji wa upatikanaji wa vitabu, uangalizi juu ya curiculum itakayoendana na karne ya 21. Uimarisha wa masomao ya sayansi, technologia, hesabu na lugha. Uanzishaji wa maabara za masomo ya sayansi. Jitihada za wizara kupunguza majukumu ya kusimamia elimu kwa kuwapa viongozi wa wilaya. Tunamatumaini serikali itazidi kutafuta mbinu imara za uongezaji wa ubora wa elimu ikishirikiana na sekta binafsi, wazazi, walimu, vyama vya walimu, wataalamu wa vyuo na halmashauri na viongozi wa kata. Jingine ni njia za uboreshwaji wa pato la mwalimu, na kuendelea kuzawadia walimu wanaonyesha uwezo bora kwa kusaidia kuongeza ubora wa elimu kwa wanafunzi.
AFYA
Bajeti ya sekta ya afya imeweza kuongezwa kutoka TSH bilion 271 mwaka 2005 na kufikia TSH trilion 1.5 mwaka huu wa fedha. Hii ni asilimia 10% ya bajeti yote ya serikali. Mikakati ya serikali katika kutoa na kuboresha huduma ya afya ni mpango wa wenye lengo la utekelezaji wa sera ya afya na mpango wa miaka kumi wa maendeleo ya msingi. Hatua hii ya serikali itasaidia kutoa huduma ya afya kwa mwananchi katika eneo la si zaidi ya kilometa tano. Ongezeko la wauguzi katika sekta ya afya. Ujenzi wa vitua vya afya katika kata na uwezo wa upatikanaji wa daktari katika kila kituo. Ujenzi wa vyuo vya mafunzo ya wahuguzi. Serikali imeweza kufanikiwa ikishirikiana na sekta binafsi katika kutoa mafunzo yenye uwezo wa upatikanaji madaktari bingwa katika hospitali nchi zima. Serikali, imeweza kutoa mafunzo ya vijana wa watanzania ndani na nje ya bara la afrika ili nchi iwe na uwezo wa kuwa na wataalamu wengi wa mambo ya afya. Mikakati ya uboreshaji wa hospitali kuanzia ngazi ya wilaya, mikoa, kanda na Hospitali ya Taifa -Muhimbilil Mikakati ya kupambana na magonjwa hatari kama vile malaria, ukwimi, kifua kikuu, mapigo ya moyo, sarakani, na vifo vya wakinamama wajawajito na watoto wenye umri usiozidi miaka mitano. Takwimu za benki ya dunia na umoja wa mataifa zinaonyesha namna gani Tanzania ilivyoweza kupunguza kasi ya magonjwa haya.


HUDUMA YA UMEME NA MAJI SAFI
Serikali imeweza kuongeza mbinu nyingine zitakazoweza kupunguza kero ya ugawo wa umeme. Serikali ya awamu ya nne imeweza kubuni vyanzo vingine kama vile gesi asilia, upepo na mionzi ya jua. Jitihada hii itaweza kutatua tatizo la kusambaza umeme kwa kutumia vyanzo vya maji.  Mfano mzuri, ni uzinduzi wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es saalam. Mradi huu utakapokamilika utaweza kuzalisha megawati 3,000 za umeme. Mradi huu utaweza kufanikiwa kuondoa umeme wa mgawo nchini.
Huduma ya utoaji maji safi vijijini na mijini umeweza kufanikiwa kwa kutoa huduma hi kwa asilimai 60% vijijini na asilimia 86% mijini. Nafikiri, changomoto kubwa ni baadhi ya maeneo ambayo hayana vyanzo vya maji na kusababisha utandikwaji wa mabomba ya kusambaza maji masafa marefu ambayo in hatua yenye gharama.
Sisi wanachama wa CCM tunapongeza juhudi za serikali katika kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa kupanga mipango imara na madhubuti na chini ya uongozi na usimamizi imara. Tunaamini uongozi unokuja utamalizia changamoto hizi za kubuni mbinu za kukabiliana nazo kwa uwezo mdogo wa serikali.
Tunaahidi kutoa ushirikiano wa bega kwa bega na viongozi wetu katika kufanya kazi kwa pamoja, bidii, mbinu mpya, umoja katika kukiboresha chama cha mapinduzi.
 Tunamatumaini makubwa na Viongozi wetu hawa imara tunaahidi tutasaidiana;
Kuendeleza kuimarisha ujenzi wa chama bora na kukiweka imara
kubuni mbinu, mikakati, utekelezaji na usimamizi ili kufikia malengo ya chama
chama kukiimarisha kijitegeme kifedha badala ya kutegemea ruzuku
Mkazo na jitihada ya kuwafikia wananchi mijini na vijijini, vijana, wanawake na wanaume na wazee
Kusaidia kutoa mawazo na mbinu kwenye jumuiya za chama na utekelezaji majukumu yake
Ukemeaji wa uchaguzi wa viongozi kwa misingi ya fedha, badala  ya uwezo, na maadili ya uongozi
Kujenga umoja ndani ya chama
Kwa kweli tunawapa Hongera kwa kuchaguliwa kuwa viongozi wa CCM katika kipindi kijacho






TUMETHUBUTU, TUMEWEZA, NA TUNASONGA MBELE

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI





IMETOLEWA NA KATIBU WA TAWI LA CCM DMV
YACOB KINYEMI
WASHINGTON DC

No comments: