


Tawi la DMV
P.O.BOX 56356 WASHINGTON DC 20040
Email
address:ccmwashdc@gmail.com
13th November, 2012
PONGEZI KWA VIONGOZI WAPYA WA
CCM TAIFA
Chama Chama Mapinduzi hapa
Marekani kinatoa pongezi kwa viongozi wapya waliochaguliwa katika mkutano Mkuu wa
CCM mjini Dodoma. Kwa niaba ya wana CCM hapa Marekani tunatoa pongezi za dhati:
MWENYEKITI WA CCM TAIFA
Mheshimiwa, Dr. jakaya Mrisho
Kikwete
MAKAMU MWENYEKITI CCM TAIFA-
TAZANIA BARA
Mheshimiwa, Philip Mangula
MAKAMU MWENYEKIT CCM TAIFA-
ZANZIBAR
Mheshimiwa, Dr. Mohamed Sheni
Mheshimiwa, Jakaya Mrisho
kikwete anaendelea kuleta misingi imara ya uongozi bora, uadilifu, ukweli,
ubunifu wa sera na usimamizi imara wa utekelezaji wa sera na itaki za chama. Kama
mwenyekiti aliyepita ameweza kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama cha
mapinduzi katika serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Juhudi za
kudumisha amani, umoja na kukemea rushwa ndani ya chama. Na kufanikiwa
kujumuisha wanachama wa rika mbali mbali na kuweza kushirikiana pamoja katika
kuboresha chama.
Mheshimiwa, Phili Mangula
anaendelea kutumikia chama akiongeza upeo wake wa siasa na itikadi, Uongozi wa
dhati na ubunifu wa siasa mpya katika mfumo huu wa vyama vingi. Mheshimiwa
mangula anaongeza uzoefu wake wa siasa na itikadi.
Mheshimiwa, Dr. Mohamedi Sheni,
akiongeza ubora na ujuzi wa uadilifu na umakini katika maamuzi.
Kwa niaba ya wanachama wote wa
CCm washio nchini Marekani tunawapongeza viongozi hawa wa ngazi ya taifa katika
kipindi kijacho.
Viongozi wote waliochaguliwa wa
NEC Tanzania bara na Zanzibar
Viongozi hawa watasaidia uwezo
wao katika kukiimarisha chama.
Shukurani zimwendee, Mheshimiwa
Jakaya Mrisho kikwete katika mipango ya mataarisho mazuri ya mkutano mkuu.
Wanachama wote wa CCM tumefarijika kuona mkutano huu unafanyika kwa njia ya
utulivu, amani, umoja, haki na upendo. Vile vile, tukitathimini utendaji wa
chama katika kipindi kilichopita tumefarijika kuona chama kimejengeka katika
misingi imara. Kubwa zaidi, wanachama wote wa chama cha mapinduzi ndani na nje
ya Tanzania tumefarijika katika hatua ya serikali ya kupanga mipango madhubuti,
kusimamia utekelezaji wake na kufikia mafanikio ya kukabiliana na changamoto
mbali mbali za maendeleo ya jamii ya wananchi na uchumi wa nchi.
Haya ni baadhi ya mafanikio ya
chama cha mapinduzi katika kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa kupitia serikali ya
jamhuri wa muungano wa Tanzania.
HALI YA UCHUMI
Katika utekelezaji wa ilani ya
uchaguzi serikali inaendelea kubabiliana na changamoto mbali mbali za maendeleo
ya uchumi wa Tanzania. Serikali iliweza kuweza kupanga mipango na usimamizi
imara juu ya mipango wa kufungua fursa kwa ukuaji uchumi, ujenzi wa mazingira
ya maendeleo ya viwanda na uimarishaji ubunifu uchumi ambao umeweza kukua kwa
asiliamia 7 mwaka 2012. Takwimu hizi zinaonyesha namna gani jinsi uchumi wa
Tanzania unavyokua kwa kasi kama nchi za India na China. Vile vile, hali hii
inaonyesha kuwa mbali na changamoto za upandaji wa bei ya gesi na matatizo ya
kiuchumi ya nchi za bara la Ulaya na Marekani lakini serikali imeweza kutafuta
mbinu na mipango ya kukuza uchumi kwa wastani wa 6% mpaka 7% kwa mwaka. Kwa
kweli lengo la serikali la ukuaji uchumi kwa 12% kwa mwaka na kuweza kuinua
hali ya maisha ya mtanzani linatia moyo. Hatua nyingine ambayo serikali imeweza
kufanikiwa ni kuongezeka kwa soko la uuzaji wa bidhaa za Tanzania nchi za nje,
hali hii imeweza kufungua mwanya wa biashara ndogo ndogo kwa wananchi. Takwimu
zinaonyesha Tanzania imeweza kuongeza Export kutoka dola za kimarekani 2,945.5
mwaka hadi kufikia dola za kimarekani 7,461.2 mwaka huu. Serikali imeweza
kuongeza akiba ya fedha za kigeni katika benki kuu kufikia dola za kimarekani
4.1, hali hii inaihakikishia moja kufikia kiwango cha kimataifa na kuiwezesha
nchi kuweza kuagiza biadha kutoka nje kwa muda takribani miezi 4. (3.8). Jingine
ni Jinsi serikali ilivyoweza kuchukua hatua za kukabiliana na upunguzaji wa
mlipuko wa bei (inflation) kutoka 19.8% na kufikia 13.5% mwaka huu. Hii ina
maana inasaidia kupunguza ukali wa maisha kwa mwananchi. Lakini, bado tunaimani
jitihada zinafanya hili kupunguza mpaka single digit (chini ya asilimia 10%) hasa katika vyakula.
MAPATO YA SERIKALI
Serikali ya awamu ya nne imeweza
kuongeza mapato ya serikali kutoka TSH. trilion 4.13 mwaka 2005/2006 mpaka
kufikia TSH. trilion 8.8. Kama
tunavyojua bajeti ya serikali ni TSH. trilion 15.2. Vile vile, hali hii
inaoshesha namna gani serikali ilivyoweza kupunguza kutegemea misaada katika
bajeti kutoka 44% mpaka 21%. Juhudi nyingine zilizoleta mafanikio ni upangaji
uzuri wa matumizi ya serikali katika bajeti ya mwaka 2012/2013 ambayo itato
kipaombele za kiipa elimu 24%, miundo mbinu 16% na afya 10% ya bajeti yote. Kwa
kweli juhudi hizi ni za kuungwa mkono kwani nchi nyingi duniani zimeweza kupiga
hatua katika maendelea ya jamii na uchumi kwa kwa kuweza kuweka fungu kubwa
katika sekta hizo. Serikali, imeweza kupata mafanikio katika kukagua matumizi
mbali mbali ya mashirika na wizara za serikali kwa kutumia ofisi ya mkaguzi
mkuu wa taasisi za serikali. Hatua hii imeweza kuwafichua wale wafanyakaji wa
umma ambao wanafuja fedha za serikali.
UWEKEZAJI
Serikali ya awamu ya nne, katika
kutekeleza ilani yake ya uchaguzi imeweza kuweka mipango na usimamizi imara wa
miradi ya gesi, viwanda, kilimo, madini na huduma ya fedha. Takwima za serikali
zinaonyesha katika mwaka 2011 kumekuwepo na miradi 826 yenye thamani ya dola za
kimarekani 7,177 na itakayoweza kutoa ajira 79,00 kwa wananchi wa Tanzania
katika kipindi kijacho.
MIUNDOMBINU
Juhudi nyingine za serikali ya
awamu ya nne ni ile kutoa kipau mbele katika uboreshwaji wa miundombinu
ardhini, majini na angani. Bajeti ya serikali ni asilimia 16%. Nchi inapoweza
kuboresha miundombinu inaweza kusaidia kupunguza gharama za usafiri, uimarishaji
wa shughuli za viwandani, kutoa mwanya ya biashara kwa wananchi wa mji mmoja na
mji mwingine. vile vile, jitihada hizi zinaweza kusaidia kuongeza kasi ya
ukuaji wa uchumi wa nchi na kuwapatia wananchi kipato katika mwanya wa kuongeza
uzalishaji wa taifa. Takwimu zinaonyesha mpaka sasa serikali inafanya jitihada
za ujenzi wa barabara za lami na za
kisasa zenye urefu wa kilometa 11,154
zinaenda kukamilika. Kwa kweli hatua hii ya serikali inastahili kuungwa mkono
kwa Tanzania na nchi ambayo inajiimarisha kwa kuwa na bara bara bora
ukilinganishwa na nchi za jirani. Mwisho, serikali imeweza kudhiirisha uwezo
mkubwa wa ujenzi kwa kutumia fedha za serikali badala ya kutegemea fedha za
wafadhili kutoka nje kwa 60% gharama zote za ujenzi na mfuko wa fedha za
barabara ( Roads fund).
ELIMU
Serikali ya awamu ya nne imeweza
kutenga 24% ya bajeti yote ya serikali katika sekta ya elimu. Hii ni hatua
nyingine muhimu ukilinganishwa na nchi nyingine katika bara la Afrika. Hatua
hii imeweza kuongeza idadi kubwa kwa watoto wenye umri wa kuingia elimu ya
msingi na kutoa huduma hii bure bila gharama. Takwimu za serikali zinaonyesha
Tanzania ni nchi pekee inayoongoza kwa asilimia 97% barani afrika kuwa na idadi
kubwa ya uandikishaji na upatikanajia wa elimu ya awali. Kwa kweli utekelezaji
huu unatia moyo kwa sababu kiwango ambacho kimewekwa na agizo la malengo ya
milenia yaliyowekwa na umoja wa Taifa in 100% itakapofika 2015. Serikali
imeweza kujenga shule za sekondari 3,165
kutoka mwaka 2005 mpaka sasa. Hatua hii ya serikali ikishirikiana na sekta
binafsi na wananchi wa kata imeweza kutoa fursa ya wanafunzi wengi kuendelea na
elimu ya sekondari. Mfano, idadi ya vijana wanaojiunga na shule za sekondari
imeongezeka kutoka wanafunzi 524,325 mwaka 2005 mpaka 1,884,272 mwaka huu. Sasa
hivi Tanzania ina idadi ya vyuo vikuu 27 nchini. Vile vile, jitihada hii
imeweza kutoa mwanya kwa wanafunzi kuendelea na elimu ya juu. Takwimu za
serikali zinaonyesha kuwa idadi imeweza kuongezeka kutoka wanafunzi 40,719 na
kufikia 166,482 hadi sasa. Serikali imeweza kupanua huduma ya utoaji wa mikopo
kwa wanafunzi ambao hawawezi kumudu gharama za elimu ya juu. Serikali ya awamu
ya nne imeweza kuongeza fedha kwa ajili ya mikopo kutoka TSH bilion 56.1 mwaka
2005 mpaka TSH bilion 306. Kisha, idadi ya wanafunzi wanaonufaika na huduma hii
imeweza kuongezeka kutoka 16,345 mpaka wanafunzi 93,176 mwaka huu. Ujenzi wa
chuo kikuu cha Dodoma ambacho kinajengwa na fedha za serikali. Ujenzi wa chuo
hichi utaweza kuchukua wanafunzi 40,000. Tunaamini, serikali bado inafanya
jitihada katika kuboresha kiwango cha elimu kinachotolewa nchi. Serikali
inaimarisha sera na viwango vya elimu ili kuweza kupima kiwango cha ubora wa
elimu ya wanafunzi. kutoa elimu ambayo italingana na makakwa ya muajiri. Ujenzi wa nyuma za walimu hasa hasa vijijini,
uimarishaji wa upatikanaji wa vitabu, uangalizi juu ya curiculum itakayoendana
na karne ya 21. Uimarisha wa masomao ya sayansi, technologia, hesabu na lugha.
Uanzishaji wa maabara za masomo ya sayansi. Jitihada za wizara kupunguza
majukumu ya kusimamia elimu kwa kuwapa viongozi wa wilaya. Tunamatumaini
serikali itazidi kutafuta mbinu imara za uongezaji wa ubora wa elimu
ikishirikiana na sekta binafsi, wazazi, walimu, vyama vya walimu, wataalamu wa
vyuo na halmashauri na viongozi wa kata. Jingine ni njia za uboreshwaji wa pato
la mwalimu, na kuendelea kuzawadia walimu wanaonyesha uwezo bora kwa kusaidia
kuongeza ubora wa elimu kwa wanafunzi.
AFYA
Bajeti ya sekta ya afya imeweza
kuongezwa kutoka TSH bilion 271 mwaka 2005 na kufikia TSH trilion 1.5 mwaka huu
wa fedha. Hii ni asilimia 10% ya bajeti yote ya serikali. Mikakati ya serikali
katika kutoa na kuboresha huduma ya afya ni mpango wa wenye lengo la
utekelezaji wa sera ya afya na mpango wa miaka kumi wa maendeleo ya msingi.
Hatua hii ya serikali itasaidia kutoa huduma ya afya kwa mwananchi katika eneo
la si zaidi ya kilometa tano. Ongezeko la wauguzi katika sekta ya afya. Ujenzi
wa vitua vya afya katika kata na uwezo wa upatikanaji wa daktari katika kila
kituo. Ujenzi wa vyuo vya mafunzo ya wahuguzi. Serikali imeweza kufanikiwa
ikishirikiana na sekta binafsi katika kutoa mafunzo yenye uwezo wa upatikanaji
madaktari bingwa katika hospitali nchi zima. Serikali, imeweza kutoa mafunzo ya
vijana wa watanzania ndani na nje ya bara la afrika ili nchi iwe na uwezo wa
kuwa na wataalamu wengi wa mambo ya afya. Mikakati ya uboreshaji wa hospitali
kuanzia ngazi ya wilaya, mikoa, kanda na Hospitali ya Taifa -Muhimbilil
Mikakati ya kupambana na magonjwa hatari kama vile malaria, ukwimi, kifua
kikuu, mapigo ya moyo, sarakani, na vifo vya wakinamama wajawajito na watoto
wenye umri usiozidi miaka mitano. Takwimu za benki ya dunia na umoja wa mataifa
zinaonyesha namna gani Tanzania ilivyoweza kupunguza kasi ya magonjwa haya.
HUDUMA YA UMEME NA MAJI SAFI
Serikali imeweza kuongeza mbinu
nyingine zitakazoweza kupunguza kero ya ugawo wa umeme. Serikali ya awamu ya
nne imeweza kubuni vyanzo vingine kama vile gesi asilia, upepo na mionzi ya
jua. Jitihada hii itaweza kutatua tatizo la kusambaza umeme kwa kutumia vyanzo
vya maji. Mfano mzuri, ni uzinduzi wa
ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es saalam. Mradi huu
utakapokamilika utaweza kuzalisha megawati 3,000 za umeme. Mradi huu utaweza
kufanikiwa kuondoa umeme wa mgawo nchini.
Huduma ya utoaji maji safi
vijijini na mijini umeweza kufanikiwa kwa kutoa huduma hi kwa asilimai 60%
vijijini na asilimia 86% mijini. Nafikiri, changomoto kubwa ni baadhi ya maeneo
ambayo hayana vyanzo vya maji na kusababisha utandikwaji wa mabomba ya
kusambaza maji masafa marefu ambayo in hatua yenye gharama.
Sisi wanachama wa CCM
tunapongeza juhudi za serikali katika kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa kupanga
mipango imara na madhubuti na chini ya uongozi na usimamizi imara. Tunaamini
uongozi unokuja utamalizia changamoto hizi za kubuni mbinu za kukabiliana nazo
kwa uwezo mdogo wa serikali.
Tunaahidi kutoa ushirikiano wa
bega kwa bega na viongozi wetu katika kufanya kazi kwa pamoja, bidii, mbinu
mpya, umoja katika kukiboresha chama cha mapinduzi.
Tunamatumaini makubwa na Viongozi wetu hawa
imara tunaahidi tutasaidiana;
Kuendeleza kuimarisha ujenzi wa
chama bora na kukiweka imara
kubuni mbinu, mikakati,
utekelezaji na usimamizi ili kufikia malengo ya chama
chama kukiimarisha kijitegeme
kifedha badala ya kutegemea ruzuku
Mkazo na jitihada ya kuwafikia
wananchi mijini na vijijini, vijana, wanawake na wanaume na wazee
Kusaidia kutoa mawazo na mbinu
kwenye jumuiya za chama na utekelezaji majukumu yake
Ukemeaji wa uchaguzi wa viongozi
kwa misingi ya fedha, badala ya uwezo,
na maadili ya uongozi
Kujenga umoja ndani ya chama
Kwa kweli tunawapa Hongera kwa kuchaguliwa
kuwa viongozi wa CCM katika kipindi kijacho
TUMETHUBUTU, TUMEWEZA, NA TUNASONGA MBELE
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
IMETOLEWA NA KATIBU WA TAWI LA
CCM DMV
YACOB KINYEMI
WASHINGTON DC
No comments:
Post a Comment