Tuesday, February 26, 2013

HEKAHEKA YA WIZI WA MAJI TANDALE MAMA ABAMBWA NA MAJI YA WIZI

 maafisa wa Dawasco wakimtoa mama huyu nyumbani kwake na kumpeleka katika gari la polisi leo 
 Mwanamke aliyetuhumiwa kuwa ni mwizi wa maji yanayosambazwa na kampuni ya Maji Safi na maji Taka  ( DAWSACO), akikamatwa eneo la Tandale jijini Dar es salaam leo wakati wa  Kampeni ya kampuni ya  DAWASCO iliyozinduliwa leo katika kupambana na watu wanaojiunganishia maji kwa wizi na kuwasambazia wateja  zake iliyoandaliwa katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani  kwa lengo la kuthibiti wizi wa asilimia 30 wa maji yanayopotea  bila ya kuwafikia wateja wak
Maama huyu anaedaiwa kwa tuhuma za wizi wa maji ya dawasco kutoboa bomba kubwa na kujaza katika tanki amelala chini akidai amezimia leo akiofia kwenda polisi

4 comments:

Anonymous said...

Treating this woman like a murderer just for water theft? Tanzania has a long way to go. Kwanza hivi kazi ya viongozi ni nini, kwa nini maji ni tatizo?

Anonymous said...

Kuna kipindi kule Masaki nyumbani kwa KINGUNGE hawa hawa maofisa walifika na kukuta amejiunganishia maji kienyeji tena kwa muda mrefu tu na sikuona vurugu pia hata kesi yenyewe sijui kama jalada lilifunguliwa na mpaka sasa kimyaaaaaaa...Waache kuwaonea wanyonge kama huko juu wanawashindwaaaa halafu hizi bunduki kama vitani maana yake nini..!!!???
PAKAJEUSI

Anonymous said...

Inasikitisha wanamzalilisha mama kwa ajili ya maji, wakati wakubwa wameiba mamilioni serikali inawaomba warudishe. kweli kwenye uhai wetu sijui kama tutaona Tanzania yenye matumaini kwa generation to come.

Anonymous said...

Duuuu!!!! hatari haikua na haja ya kuleta waandishi kwa kituko hiko kumdhalilisha huyu mama,,, heee nyie mambo ya muhimu hamuyafuatilii munafuatilia ujinga kama huu hata mimi ningeunganisha maji ikiwa maji taabu mtu afanyeje? aaahhh!!!! mamilioni yetu yameibwa kimya mpaka leo tunapigwa change la macho!!! na ndo hao hao wanaozitoa kujidai wanatoa misaada kumbe wanataka wachaguliwe urais ili wazidi kujinufaisha katika haya maisha mafupi ya kupita,, lakini ole wao watajiju siku ambayo kitadhihirishwa kila kitu,,, feel sorry mama wa watu... aahh!!! TANZANIA MBOVU ILIOJAA UDHALIMU NA UHASIDI...