Tuesday, February 26, 2013

SHEREHE ZA MIAKA 3 YA VIJIMAMBO NA TAMASHA LA UTAMADUNI WA KISWAHILI MAREKANI YA KASKAZINI

Blog ya Vijimambo ikishirikiana na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani  na Mexico na Jumuiya ya Watanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia wanapanga kusheherekea miaka 3 ya Vijimambo kwa kuendeleza Lugha na Utamaduni wa Kiswahili. Madhumuni ya hili tamasha ni kuendeleza lugha na utamaduni wa Kiswahili hapa Marekani ya Kaskazini ili watoto wanaoishi huku Marekani ya Kaskazini waweze kuendeleza matumizi ya lugha hii na utamaduni wake kizazi hadi kizazi. 

July 6, 2013  hapa DMV kwenye Hall la Hampton Conference Center lililopo 
207 w Hampton Pl, 
Capitol Height, MD

Mambo mengi yatakuwepo, Vikundi mbalimbali vya utamaduni, vyakula vya Kitanzania, Wasanii kutoka nyumbani na hapa Marekaniyote ni kudumisha utamaduni wa kiswahili Marekani ya Kaskazini

TEGA SIKIO HABARI ZAIDI ZITAFUATA
-------------------------------------------------------
kwa wajasiliamali ambao wangepenga kudhamini na kuijipatia meza ya kutangaza bidhaa au shughuli wazifanyazo tafadhali wasiliana 301 613 5165 Asante

No comments: