ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, March 24, 2013

DARASA LA KUJIFUNZA LUGHA YA KISWAHILI SIKU YA KWANZA LILIVYOAANZA, DMV


Video ya Darasa la Kiwsahili lilivyoanza na walimu walivyokua wakiwafahamu wtaoto uwezo wao na baadhi ya watoto wakijaribu kufanya mahojiano kwa kiswahili na mtangazaji wetu wa Vijimambo Abdulhamani. Hebu WASIKILIZE

6 comments:

Anonymous said...

Hii ni hatua nzuri sana, mimi ni mwalimu wa lugha by profession na nadhani nitakuwa tayari kuwasaidia maana kufundisha lugha nako sio rahisi kama watu wanavyodhani. Kwa mfano sio lazima kufundisha mtoto mmoja mmoja itawachukua muda mwingi ila kunambinu nyingine za kiualimu ambazo unaweza kutumia na ukawafanya watoto kuelewa lugha haraka. Nitawasliliana nanyi ili nijue jinsi ya kuweza kusaidia pia.Ila mwanzo ni mzuri sana hongereni

Anonymous said...

wewe mwalimu umekaa mtoto kasimama ni ndiyo ni nini idea nzuri lakini mwalimu ka kaa chini oooh noo

Anonymous said...

Hapo juu, hii ni siku ya kwanza ya walimu kukutana na wanafuninzi na ni lazima wafanyiwe personal evaluation ili waweze kupangwa kwa levels ya kuelewa kiswahili; kama unavyoona wengine wanajua kuongea, wengine wanasikia na hawajui kuongea wengine hawasikii wala kuongea kiswahili. Hili darasa litakuwa linafundishwa kwa groups kutokana na evaluation waliyofanyiwa kwenye hii video. Na ni kitu cha kawaida katika kujifunza lugha yeyote. JOB WELL DONE DMV leadership

Anonymous said...

Hili ni wazo zuri sana. Ila ningeshauri kupata ushauri wa Watanzania waliokwenda vyuoni katika nchi ambazi haziongei Kiswahili/ Kiingereza. Kwa mfano utagundua kuwa haitakiwi kumfundisha mtu lugha moja kwa kumwuliza au kumwelekeza kutumia lugha ingine ambayo anaijua. Msiwafundishe kiswahili kwa kutumia kiingereza kuulizia maswali.

Anonymous said...

Kweli mwanzo mzuri. Kazi itakuwa ya ufanisi mkubwa incase walimu profesional watafanya. Lakini popote penyebure, ufanisi ktk ubora utakuwa mdogo. Mkitaka kazi ifanyike kwa viwango vyenye mafanikio gharimieni. Also this is not intertainment, wazazi wamepeleka watoto kama tour ya park fulani. Mtoto ili aelewe anatakiwa awe mbali na mlezi/guardian wake.

Anonymous said...

Job well done...ila na sisi watz wakubwa tujifunze kiswahili na tuwe fasaha tusiwachanganye watoto... haba na haba ni kidogo kidogo siyo nusu nusu.