Kisaka, kipa wa zamani wa Volcano ya Kenya amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa unaosababisha mwili wake kukosa nguvu upande mmoja ingawa mwenyewe amesema si kupooza kama ilivyoelezwa awali.
Amekuwa akiendelea na matibabu, hata hivyo, Kisaka alilalama kushindwa kuhimili gharama kubwa ya matibabu hivyo kuwaomba wadau wajitokeze kumsaidia.
Championi likachukua nafasi ya kuomba wadau wajitokeze kumsaidia lakini uamuzi ukawa ni kuanza kuwa mfano kwa kutoa angalau kiasi cha fedha ili kuwahamasisha wadau kumsaidia Kisaka ambaye hata kutembea, analazimika kusaidiwa.
PICHA NA WILBERT MOLANDI.
No comments:
Post a Comment