Advertisements

Sunday, December 15, 2013

OKWI ASAINI YANGA MIAKA MIWILI NA NUSU, TEAM HATA UWANJA WA MAZOEZI HAINA TUTAFIKA KWELI YADAIWA ML 180 ZA TUMIKA KUPATA SIGN YAKE


 Emmanuel Okwi amesaini Yanga kwa miaka miwili.

Yanga imemsainisha kwa miaka miwili na Bin Kleb AMETHIBITISHA.
Tayari ITC ya Okwi imetua maana yake sasa ni mchezaji halali wa Yanga. Yale yale yakumwaga mapesa kwa wachezaji wageni wakati timu inakosa hata uwanja wa mazoezi.
Mwezi sasa toka mwenyekiti wa team Manji ametangaza kuachia ngazi  licha ya kumwaga mapesa mala kwa mala kwa wachezaji. Sasa nini kitafata  ni uomba omba wa kutembeza mfuko wa rambo kuomba misaada?. Viongozi waliingia madarakani baada ya kuwahadaa wapiga kura kuwa watajenga uwanja wa kisasa na michoro ya uwanja huo ikawekwa bayana. Lakini leo hii akuna hata kifusi cha kuanza kwa uwanja huo na Manji aliekuwa ameiingia madaraka kwa njia hiyo ametangaza kuachia ngazi je anaekuja atakuja na sera gani?. Au wataendelea na usemi wa Yanga Imara Daima?. Kwanini hao akina Kleb na Manji wasiungane na kujenga uwanja  wa kisasa kama kitega uchumi cha team kama kweli wana mapenzi mema ya kimaendeleo katika team?.

1 comment:

Kombo said...

huu wako ni uchochezi kwa klabu ya yanga. unataka nini?. uwanja tutajenga tu. kwani simba waliosaini hamis tambwe, owino, ivo na wengine uwanja wao uko wapi. Inonekana umeumwa sana na kitendo cha Okwi kusaini yanga. hilo ndio soka la sasa mzee amka.

Tuache

manyu Zanzibar