Advertisements

Thursday, May 29, 2014

GALA DINNER YA AFRICAN DAY WASHINGTON, DC YAFANA SANA, MEYA WA DC NDANI YA NYUMBA, TANZANIA NA RWANDA NDIO WAANDAAJI WA MWAKA HUU



Balozi wa kudumu wa African Union Mhe. Amina Salum Ali akiwa kwenye gwaride la bendera wakati hafla ya gala dinner ya African Day iliyofanyika Washington, DC siku ya Jumanne May 27, 2014 katika hotel ya Marriott na kuhudhuriwa na watu zaidi ya 2,000. Afriacam day ya mwaka huu iliandaliwa na Ubalozi wa Tanzania wakishirikiana na Ubalozi wa  Rwanda

Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula akiwa kwenye gwaride la bendera wakati wa ufunguzi wa Gala dinner ya African Day siku ya Jumanne May 27, 2014 katika hotel ya Marriott, Washington, DC.



Mabalozi wakisimama kwa nyimbo za taifa za Marekani na African Union.

Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula akitoa hotuba ya kuwakaribisha wageni siku ya Jumanne May 27, 2014 siku ya African day iliyoadhimishwa Marriott ya Washington, DC.

Balozi wa Rwanda nchini Marekani Mhe.Mathilde Munkanabana nae akitoa hotuba ya kuwakaribisha wageni.

Balozi wa kudumu wa African Union, Mhe. Amina Salum Ali akitoa hotuba.

Meya wa DC, Mhe.Vincent Gray akitoa hotuba.

Meya wa DC, Mhe. Vinceny Gray akimkabidhi hati ya baraza la jiji la DC Balozi wa kudumu wa African Union, Mhe. Amina Salum Ali ya Jiji la Washington, DC kutambua rasmi siku ya African Day.

Meya katika picha ya pamoja na waheshimiwa Mabalozi wa Rwanda, Tanzania na African Union.

Mwakilishi wa Serikali ya Marekani Mhe. Linda Thomas Greenfield akitoa hotuba.
Video ya dance ya African Day
kwa picha zaidi bofya soma zaidi


Mhe. Linda Thomas Greenfield katika picha ya pamoja na waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania na Rwanda.

Balozi wa DRC nchini Marekani Mhe. Faida Mitifu akisoma wasifu wa msemaji mkuu wa Afriacan Day Dr. Juma Calestous ambaye ni profesa, Harvard Kennedy School of Gevernment.

Msemaji mkuu wa African Day Dr. Juma Calestous akitoa hotuba yake.

Dr. Juma Colestous katika picha ya pamajoa na waheshimiwa Mabalozi.

Balozi wa Ivory Coast, Mhe. Douda Diabate akitoa hotuba.
Balozi wa Rwanda akisalimia na wageni wakati wa Cocktail Reception.
Balozi wa Tanzania akisalimiana na wageni wakati wa Cocktail Reception.
Picha ya pamoja.

 Kikundi cha utamaduni kutoka Zimbabwe kikitumbuiza kwenye Gala Dinner ya African Day iliyofanyuka siku ya Jumanne May 27, 2014, Marriott Washington, DC.
Juu na chini ni viikundi cha utamaduni kutoka Rwanda kikitoa burudani kwenye siku ya Gala dinner ya Africa Day.
Mhe Balozi Liberata Mulamula Balozi wa Tanzania nchini Marekani akijumuika kwenye ngoma ya utamaduni ya kikundi toka Rwanda.
Mhe. Balozi Mathilde Mukatabana (kati) Balozi wa Rwanda nchini Marekani akijumuika na kikundi cha utamaduni kutoka Rwanda kilipokua kikitoa burudani kwenye Gala dinner ya African Day.


1 comment:

Anonymous said...

Nina swali hivi shuguli kama hizi Ubalozi wetu tena walikuwa mahost wanatumia vigezo gani kuwaalika watanzania wakazi wa hapa DMV?? Ukiacha viongozi wa jumuiya. Lazima kuwe na system itakayofanya kila mtanzania ashiriki shuguli zinazohusu nchi yetu. Watanzania wengi tumejiandikisha ubalozini kwa nini pasiwe na list mfano akija Rais Kikwete anataka kuonana na watanzani wachache they can go to the list pick 1st 50 na kuwatumia email kuwataarifu, ikitokea event nyingine the next 50 wanaalikwa. Ili kila mtanzania apewe nafasi ya kushiriki sio mpaka uwe na mjomba shangazi au rafiki ubalozini ndiyo wale wale wanaonekana kwenye shuguli za kuhusisha nchi yetu.. NI MAWAZO TUU.