Thursday, May 29, 2014

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Amtembelea Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai, Ifisini kwake

Mheshimiwa Omar Mjenga, Balozi Mdogo wa Ubalozi wa Tanzania uliopo Dubai, akiwa na mazungumzo na Ndugu Nehemiah Mchechu, Mkurugenzi Mkuu wa NHC , alipomtembelea Ofisini kwake Dubai.

Mazungumzo yao yalihusu maandalizi ya kongamano la uwekezaji katika sekta ya nyumba litakalofanyika Jumeirah Madnat Hotel, Dubai. Kongamano hilo limeandaliwa na Ubalozi Mdogo wa Tanzania uliopo Dubai kwa kushirikiana na Shirika la Taifa la Nyumba (NHC).

Makampuni makubwa ya sekta ya nyumba hapa Dubai pamoja na mengine kutoka Nchi za Muungano wa Ukanda wa Mashariki ya Kati (GCC and the Midle East) yatashiriki. Makumpuni hayo ni pamoja na Nakheel ambalo ndio limejenga The Palm City ya Dubai, Emaar ambalo ndio wamiliki wa Dubai Mall. Mengine yanatoka Qatar, Bahrain, Oman na Saudi Arabia.

No comments: