
Ofisi ya Makamu wa Rais
(Mazingira), imetunga kanuni ya kudhibiti kelele na mitetemo kutoka kwa
waendeshaji wa klabu za usiku, baa, matangazo ya wanaozunguka barabarani
na hata mahubiri katika maeneo ya ibada.
Kwa sasa kanuni hiyo
iko kwa Mchapishaji Mkuu wa Serikali na tayari imesainiwa na
Waziri
anayeshughulikia Mazingira. Kadhalika wananchi wametakiwa kutoa taarifa
za kero zitokanazo na maeneo hayo ya biashara kwani yamekuwa yakichangia
kuporomosha maadili ya taifa.
Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji kutoka Baraza la Mazingira
nchini (NEMC), Dk Robert Ntakamulenga alisema hayo jana Dar es Salaam
wakati akizungumzia kero ambazo wananchi wamezifikisha ofisini kwake.
“Kama unapiga kelele inayozidi kiwango cha desbell 45 inahitajika kibali na kelele za aina hiyo ni zile zinazoanzia saa moja asubuhi hadi saa nne usiku iwe mwisho,” alisema na kuongeza baa ambazo zinapiga kelele za aina hiyo hadi usiku zinavunja sheria,” alisema Ntakamulenga.
“Kama unapiga kelele inayozidi kiwango cha desbell 45 inahitajika kibali na kelele za aina hiyo ni zile zinazoanzia saa moja asubuhi hadi saa nne usiku iwe mwisho,” alisema na kuongeza baa ambazo zinapiga kelele za aina hiyo hadi usiku zinavunja sheria,” alisema Ntakamulenga.
1 comment:
Saws kabisa nakubaliana na hilibswala ni mujimu sana kwabkuwapa fursa watu kutulizana mawazo na pressure za kazi na foleni. Itifaki izingatiwe.
Post a Comment