SISTA
wa Parokia ya Makoka iliyopo Kibangu, Dar ameuawa na majambazi
yaliyokuwa kwenye bodoboda wakati akiingia kwenye gari akitokea dukani
eneo la River Side, Ubungo jijini Dar es Salaam hivi punde.
Kabla ya kuuawa sista huyo, dereva wake alipigwa risasi mkononi na majambazi hayo.Chanzo GPL
5 comments:
Majambazi au Alshabab. Ingelikua Zanzibar mungelikwisha mfunga paka kengele. Kunya anye kuku akinya bata kahara. Tuweni pole sana.
Haya tupeni taarifa ya serikali inasema nn kuhusu janga hili? Au ndo wanakaa kimya, kama walivyofanya kwenye ajali ya makongo juzi! !? Cjui hawa viongoz wetu wana elimu ya wapiii? Kazi ni majungu tuu bungeni na ufisadi..kazi hawafanyi kabisaaa, inatia uchungu sana nchi yetu , viongoz wetu wote akili ziko kwenye totoz tuuu, yaani wanapewa mishahara ya bureee! !!!
Hakika mwanadamu alie hai acha nae kwani hatabirki.Damu yake na iwe juu ya watu hao pia ndiyo wa wao kuiba takawasitake hawataua tena mtu mwingine!Mungu Baba yetu mtoa hukumu iliyohaki uipokee roho ya sista huyo na umponyeshe dereva na umpe Amani yako ipitayo amani zote!
Nchi hii imejaa amani tele sasa sijui amani hii ni ipi?leo hii wezi,majambazi haya yamo humu humu nchini wala haya adhibiwi tena yanawatetezi yakifungwa kidogo yako nje na yanajitapa.Ukweli ni kwamba vyombo vya sheria fanyeni kazi na muogopeni MUNGU wala si mwanadamu ye yote awae hai au marehemu,tunaelekea pabaya mnoooo!!!!!!!! watu wanatembea na silaha kama mchezo hakuna upekuzi wa kina kwa watu wote na saa zote,kwani maaskari wangekaa huko mitaani na mabarabarani wakipekuwa watu bila kujali ni nani wakati gani kwa nini watu wamesimama hovyo hovyo pia magari na mapiki piki haya yakaguliwe kila saa na sehemu zote maaskari acheni kushinda vituoni!
Tanzania sasa imeharibika kila mtu anarisasi .then wanakubali waamiaji wamekuwa wengi .ndio wanaingia na bastola.maskini sistar mungu amlaze ,ahali pema poponi.
Post a Comment